Jonah 2
1Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
2Akasema: 1 “Katika shida yangu nalimwita Bwana, 2 naye akanijibu. 1 Kutoka kina cha kaburi + 2:2 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. niliomba msaada, 2 nawe ukasikiliza kilio changu. 1
3Ulinitupa kwenye kilindi, 2 ndani kabisa ya moyo wa bahari, 2 mikondo ya maji ilinizunguka, 1 mawimbi yako yote na viwimbi 2 vilipita juu yangu. 1
4Nikasema, ‘Nimefukuziwa 2 mbali na uso wako, 1 hata hivyo nitatazama tena 2 kuelekea Hekalu lako takatifu.’ 1
5Maji yaliyonimeza yalinitisha, 2 kilindi kilinizunguka; 2 mwani + 2:5 Mwani hapa maana yake ni magugu yaotayo kwenye sakafu ya kilindi cha bahari. ulijisokota kichwani pangu. 1
6Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, 2 makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. 1 Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, 2 Ee Bwana Mungu wangu. 1
7“Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, 2 nilikukumbuka wewe, Bwana, 1 nayo maombi yangu yalikufikia wewe, 2 katika Hekalu lako takatifu. 1
8“Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa 2 hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao. 1
9Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, 2 nitakutolea dhabihu. 1 Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. 2 Wokovu watoka kwa Bwana.”
10Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.