Ecclesiastes · Biblia (Kiswahili)

Ecclesiastes 10

1Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, 2 ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima. 1

2Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, 2 lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto. 1

3Hata anapotembea barabarani, 2 mpumbavu hukosa ufahamu 1 na kudhihirisha kwa kila mmoja 2 jinsi alivyo mpumbavu. 1

4Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, 2 usiache mahali pako, 2 utulivu huweza kuzuia makosa mengi. 1

5Kuna ubaya niliouona chini ya jua, 2 aina ya kosa litokalo kwa mtawala: 1

6Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, 2 wakati matajiri hushika nafasi za chini. 1

7Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, 2 wakati wakuu wakitembea 2 kwa miguu kama watumwa. 1

8Yeye achimbaye shimo 2 aweza kutumbukia ndani yake, 1 yeyote abomoaye ukuta 2 anaweza kuumwa na nyoka. 1

9Yeyote apasuaye mawe 2 inawezekana yakamuumiza, 1 yeyote apasuaye magogo 2 inawezekana yakamuumiza. 1

10Kama shoka ni butu 2 na halikunolewa, 1 nguvu nyingi zinahitajika, 2 lakini ustadi utaleta mafanikio. 1

11Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, 2 mwaguzi hatahitajika tena. 1

12Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima 2 yana neema, 2 bali mpumbavu huangamizwa 2 na midomo yake mwenyewe. 1

13Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, 2 mwishoni ni wazimu mbaya, 2

14naye mpumbavu huzidisha maneno. 1 Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, 2 ni nani awezaye kueleza ni jambo gani 2 litakalotokea baada yake? 1

15Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, 2 hajui njia iendayo mjini. 1

16Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa 2 na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi. 1

17Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika 2 na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: 2 ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi. 1

18Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, 2 kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja. 1

19Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, 2 nao mvinyo hufurahisha maisha, 2 lakini fedha ni jawabu la mambo yote. 1

20Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, 2 au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, 1 kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, 2 naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.

← Ecclesiastes 9Read In The App, Free →Ecclesiastes 11 →

Study Ecclesiastes 10

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112