Ecclesiastes · Biblia (Kiswahili)

Ecclesiastes 7

1Afadhali sifa nzuri kuliko manukato safi, 2 nayo siku ya kufa kuliko ya kuzaliwa. 1

2Afadhali kwenda kwenye nyumba ya msiba 2 kuliko kwenda kwenye nyumba ya karamu, 1 kwa kuwa kifo ni hatima ya kila mwanadamu, 2 imewapasa walio hai kuliweka hili mioyoni mwao. 1

3Huzuni ni afadhali kuliko kicheko, 2 kwa sababu uso wenye huzuni wafaa kwa moyo. 1

4Moyo wa wenye hekima uko katika nyumba ya msiba, 2 lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya anasa. 1

5Afadhali kusikia karipio la mtu mwenye hekima, 2 kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu. 1

6Kama ilivyo kuvunjika kwa miiba chini ya sufuria, 2 ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu. 2 Hili nalo pia ni ubatili. 1

7Dhuluma humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu, 2 nayo rushwa huuharibu moyo. 1

8Mwisho wa jambo ni bora kuliko mwanzo wake, 2 uvumilivu ni bora kuliko kiburi. 1

9Usiwe mwepesi kukasirika rohoni mwako, 2 kwa kuwa hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu. 1

10Usiseme, “Kwa nini siku za kale zilikuwa bora kuliko siku hizi?” 2 Kwa maana si hekima kuuliza maswali kama hayo. 1

11Hekima, kama ulivyo urithi, ni kitu chema 2 na huwafaidia wale walionalo jua. 1

12Hekima ni ulinzi kama fedha ilivyo ulinzi, 2 lakini faida ya maarifa ni hii: 2 kwamba hekima huhifadhi maisha ya aliye nayo.

13Tafakari kile Mungu alichokitenda: 1 Nani awezaye kunyoosha 2 kile ambacho yeye amekipinda? 1

14Nyakati zikiwa nzuri, ufurahi, 2 lakini nyakati zikiwa mbaya, tafakari: 1 Mungu amefanya hiyo moja, 2 naam, sanjari + 7:14 Sanjari hapa maana yake mwandamano wa vitu, wanyama au watu. na hiyo nyingine. 1 Kwa hiyo, mwanadamu hawezi kugundua 2 kitu chochote kuhusu maisha yake ya baadaye.

15Katika maisha haya yangu ya ubatili nimeshaona haya mawili: 1 mtu mwadilifu akiangamia katika uadilifu wake, 2 naye mtu mwovu akiishi maisha marefu katika uovu wake. 1

16Usiwe mwenye haki kupita kiasi, 2 wala usiwe na hekima kupita kiasi: 2 kwa nini kujiangamiza mwenyewe? 1

17Usiwe mwovu kupita kiasi, 2 wala usiwe mpumbavu: 2 kwa nini kufa kabla ya wakati wako? 1

18Ni vyema kushika hilo moja 2 na wala usiache hilo jingine likupite. 2 Mtu amchaye Mungu ataepuka huko kupita kiasi. + 7:18 Au: atafuata hayo yote mawili. 1

19Hekima humfanya yeye aliye nayo kuwa na uwezo zaidi 2 kuliko watawala kumi katika mji. 1

20Hakuna mtu mwenye haki duniani 2 ambaye hufanya mambo ya haki 2 na kamwe asitende dhambi. 1

21Usitie maanani kila neno linalosemwa na watu, 2 la sivyo, waweza kumsikia 2 mtumishi wako akikulaani: 1

22kwa kuwa unafahamu moyoni mwako 2 kwamba wewe mwenyewe mara nyingi 2 umewalaani wengine.

23Yote haya niliyajaribu kwa hekima, nikasema, 1 “Nimeamua kuwa na hekima”: 2 lakini hii ilikuwa nje ya uwezo wangu. 1

24Vyovyote hekima ilivyo, 2 hekima iko mbali sana na imejificha, 2 ni nani awezaye kuigundua? 1

25Nikageuza fikira zangu ili kuelewa, 2 kuchunguza na kuitafuta hekima 2 na kusudi la mambo, 1 na ili kuelewa ujinga wa uovu, 2 na wazimu wa upumbavu. 1

26Nimeona jambo lililo chungu kuliko mauti, 2 mwanamke ambaye ni mtego, 1 ambaye moyo wake ni wavu wa kutegea 2 na mikono yake ni minyororo. 1 Mtu ampendezaye Mungu atamkwepa, 2 bali mwenye dhambi atanaswa naye.

27Mhubiri anasema, “Tazama, hili ndilo nililogundua: 1 “Nimegundua kitu kimoja baada ya kingine nilipokuwa katika kusudi la mambo: 2

28ningali natafiti 2 lakini sipati: 1 nilimpata mwanaume mmoja mnyofu miongoni mwa elfu, 2 lakini hakuna mwanamke mmoja mnyofu miongoni mwao. 1

29Hili ndilo peke yake nililolipata: 2 Mungu amemuumba mwanadamu mnyofu, 2 lakini mwanadamu amebuni mambo mengi.”

← Ecclesiastes 6Read In The App, Free →Ecclesiastes 8 →

Study Ecclesiastes 7

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112