Joel · Biblia (Kiswahili)

Joel 1

1Neno la Bwana ambalo lilimjia Yoeli mwana wa Pethueli. 1 Uvamizi Wa Nzige 1

2Sikilizeni hili, enyi wazee; 2 sikilizeni, ninyi nyote mnaoishi katika nchi. 1 Je, jambo kama hili lilishawahi kutokea 2 katika siku zenu au katika siku za babu zenu? 1

3Waelezeni watoto wenu, 2 na watoto wenu wawaambie watoto wao, 2 na watoto wao kwa kizazi kitakachofuata. 1

4Kilichosazwa na kundi la tunutu 2 nzige wakubwa wamekula, 1 kilichosazwa na nzige wakubwa 2 parare wamekula, 1 kilichosazwa na parare 2 madumadu wamekula. 1

5Amkeni, enyi walevi, mlie! 2 Pigeni yowe enyi wanywaji wote wa mvinyo, 1 pigeni yowe kwa sababu ya mvinyo mpya, 2 kwa kuwa mmenyangʼanywa 2 kutoka midomoni mwenu. 1

6Taifa limevamia nchi yangu, 2 lenye nguvu tena lisilo na idadi; 1 lina meno ya simba, 2 magego ya simba jike. 1

7Limeharibu mizabibu yangu 2 na kuangamiza mitini yangu. 1 Limebambua magome yake 2 na kuyatupilia mbali, 2 likayaacha matawi yake yakiwa meupe. 1

8Omboleza kama bikira aliyevaa nguo ya gunia 2 anayehuzunika kwa ajili ya mume wa ujana wake. 1

9Sadaka za nafaka na sadaka za kinywaji 2 zimekatiliwa mbali kutoka nyumba ya Bwana. 1 Makuhani wanaomboleza, 2 wale wanaohudumu mbele za Bwana. 1

10Mashamba yameharibiwa, 2 ardhi imekauka; 1 nafaka imeharibiwa, 2 mvinyo mpya umekauka, 2 mafuta yamekoma. 1

11Kateni tamaa, enyi wakulima, 2 lieni, enyi mlimao mizabibu; 1 huzunikeni kwa ajili ya ngano na shayiri, 2 kwa sababu mavuno ya shambani yameharibiwa. 1

12Mzabibu umekauka 2 na mtini umenyauka; 1 mkomamanga, mtende na mtofaa, 2 miti yote shambani, imekauka. 1 Hakika furaha yote ya mwanadamu 2 imeondoka. 1 Wito Wa Toba 1

13Vaeni nguo ya gunia, enyi makuhani, muomboleze; 2 pigeni yowe, enyi mnaohudumu madhabahuni. 1 Njooni, vaeni nguo ya gunia usiku kucha, 2 enyi mnaohudumu mbele za Mungu wangu; 1 kwa kuwa sadaka za nafaka na sadaka za kinywaji 2 zimezuiliwa kufika katika nyumba ya Mungu wenu. 1

14Tangazeni saumu takatifu; 2 liiteni kusanyiko takatifu. 1 Iteni wazee 2 na wote waishio katika nchi 1 waende katika nyumba ya Bwana Mungu wenu, 2 wakamlilie Bwana. 1

15Ole kwa siku hiyo! 2 Kwa kuwa siku ya Bwana iko karibu; 1 itakuja kama uharibifu 2 kutoka kwa Mwenyezi. + 1:15 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania. 1

16Je, chakula hakikukatiliwa mbali 2 mbele ya macho yetu: 1 furaha na shangwe 2 kutoka nyumba ya Mungu wetu? 1

17Mbegu zinakauka 2 chini ya mabonge ya udongo. 1 Ghala zimeachwa katika uharibifu, 2 ghala za nafaka zimebomolewa, 2 kwa maana hakuna nafaka. 1

18Jinsi gani ngʼombe wanavyolia! 2 Makundi ya mifugo yanahangaika 1 kwa sababu hawana malisho; 2 hata makundi ya kondoo yanateseka. 1

19Kwako, Ee Bwana, naita, 2 kwa kuwa moto umeteketeza 2 malisho ya mbugani 1 na miali ya moto imeunguza 2 miti yote shambani. 1

20Hata wanyama wa porini wanakuonea shauku; 2 vijito vya maji vimekauka, 1 na moto umeteketeza 2 malisho yote ya mbugani.

← Hosea 14Read In The App, Free →Joel 2 →

Study Joel 1

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123