Jeremiah 47
1Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajaishambulia Gaza:
2Hili ndilo asemalo Bwana: 1 “Tazama jinsi maji yanavyoinuka huko kaskazini, 2 yatakuwa mafuriko yenye nguvu sana. 1 Yataifurikia nchi na vitu vyote vilivyomo ndani yake, 2 miji na wale waishio ndani yake. 1 Watu watapiga kelele; 2 wote waishio katika nchi wataomboleza 1
3kwa sauti ya kwato za farasi waendao mbio, 2 kwa sauti ya magari ya adui 2 na mngurumo wa magurudumu yake. 1 Baba hawatageuka kuwasaidia watoto wao, 2 mikono yao italegea. 1
4Kwa maana siku imewadia 2 kuwaangamiza Wafilisti wote 1 na kuwakatilia mbali walionusurika wote 2 ambao wangeweza kusaidia Tiro na Sidoni. 1 Bwana anakaribia kuwaangamiza Wafilisti, 2 mabaki toka pwani za Kaftori. + 47:4 Kaftori ndio Krete. 1
5Gaza atanyoa kichwa chake katika kuomboleza, 2 Ashkeloni atanyamazishwa. 1 Enyi mabaki kwenye tambarare, 2 mtajikatakata wenyewe mpaka lini? 1
6“Mnalia, ‘Aa, upanga wa Bwana, 2 utaendelea mpaka lini ndipo upumzike? 1 Rudi ndani ya ala yako; 2 acha na utulie.’ 1
7Lakini upanga utatuliaje 2 wakati Bwana ameuamuru, 1 wakati ameuagiza kuishambulia Ashkeloni 2 pamoja na pwani yake?”