Micah 1
1Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu. 1
2Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, 2 sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, 1 ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, 2 Bwana kutoka Hekalu lake takatifu. 1 Hukumu Dhidi Ya Samaria Na Yerusalemu 1
3Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; 2 anashuka na kukanyaga 2 mahali palipoinuka juu pa dunia. 1
4Milima inayeyuka chini yake 2 na mabonde yanagawanyika 1 kama nta mbele ya moto, 2 kama maji yatiririkayo kasi 2 kwenye mteremko. 1
5Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, 2 ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. 1 Kosa la Yakobo ni lipi? 2 Je, sio Samaria? 1 Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? 2 Je, sio Yerusalemu? 1
6“Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, 2 mahali pa kuotesha mizabibu. 1 Nitayamwaga mawe yake katika bonde 2 na kuacha wazi misingi yake. 1
7Sanamu zake zote 2 zitavunjwa vipande vipande; 1 zawadi zake zote za Hekalu 2 zitachomwa kwa moto; 2 nitaharibu vinyago vyake vyote. 1 Kwa kuwa alikusanya zawadi zake 2 kutokana na ujira wa kahaba, 1 nazo zitatumika tena 2 kulipa mishahara ya kahaba.” 1 Kulia Na Kuomboleza 1
8Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; 2 nitatembea bila viatu na tena uchi. 1 Nitabweka kama mbweha 2 na kuomboleza kama bundi. 1
9Kwa sababu jeraha lake halitibiki; 2 limekuja Yuda. 1 Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, 2 hata Yerusalemu kwenyewe. 1
10Usiliseme hili huko Gathi; 2 usilie hata kidogo. 1 Huko Beth-le-Afra 2 gaagaa mavumbini. 1
11Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, 2 ninyi mkaao Shafiri. 1 Wale waishio Saanani 2 hawatatoka nje. 1 Beth-Eseli iko katika maombolezo; 2 kinga yake imeondolewa kwako. 1
12Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu 2 wakingoja msaada, 1 kwa sababu maangamizi yamekuja 2 kutoka kwa Bwana, 2 hata katika lango la Yerusalemu. 1
13Enyi mkaao Lakishi, 2 fungeni farasi kwenye magari ya vita. 1 Mlikuwa chanzo cha dhambi 2 kwa Binti Sayuni, 1 kwa kuwa makosa ya Israeli 2 yalikutwa kwako. 1
14Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi 2 zawadi za kuagana. 1 Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu 2 kwa wafalme wa Israeli. 1
15Nitawaleteeni atakayewashinda 2 ninyi mnaoishi Maresha. 1 Yeye aliye utukufu wa Israeli 2 atakuja Adulamu. 1
16Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza 2 kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; 1 jifanyieni upara kama tai, 2 kwa kuwa watawaacha 2 na kwenda uhamishoni.