Micah 2
1Ole kwa wale wapangao uovu, 2 kwa wale wafanyao shauri la hila vitandani mwao! 1 Kunapopambazuka wanalitimiza 2 kwa sababu uko katika uwezo wao kutekeleza. 1
2Wanatamani mashamba na kuyakamata, 2 pia nyumba na kuzichukua. 1 Wanamlaghai mwanaume nyumba yake, 2 mwanadamu mwenzake urithi wake.
3Kwa hiyo, Bwana asema: 1 “Ninapanga maangamizi dhidi ya watu hawa, 2 ambayo hamwezi kujiokoa wenyewe. 1 Hamtatembea tena kwa majivuno, 2 kwa kuwa utakuwa ni wakati wa maafa. 1
4Siku hiyo watu watawadhihaki, 2 watawafanyia mzaha 2 kwa wimbo huu wa maombolezo: 1 ‘Tumeangamizwa kabisa; 2 mali ya watu wangu imegawanywa. 1 Ameninyangʼanya! 2 Ametoa mashamba yetu kwa wasaliti.’ ” 1
5Kwa hiyo hutakuwa na yeyote katika kusanyiko la Bwana 2 wa kugawanya mashamba kwa kura. 1 Manabii Wa Uongo 1
6Manabii wao husema, “Usitabiri. 2 Usitabiri kuhusu vitu hivi; 2 aibu haitatupata.” 1
7Je, ingesemwa, ee nyumba ya Yakobo: 2 “Je, Roho wa Bwana amekasirika? 2 Je, yeye hufanya vitu kama hivyo?” 1 “Je, maneno yangu hayamfanyii mema 2 yeye ambaye njia zake ni nyofu? 1
8Siku hizi watu wangu wameinuka 2 kama adui. 1 Unawavua joho la kitajiri wale wanaopita 2 pasipo kujali, 2 kama watu warudio kutoka vitani. 1
9Unawahamisha wanawake wa watu wangu 2 kutoka kwenye nyumba zao za kupendeza. 1 Unaondoa baraka yangu 2 kwa watoto wao milele. 1
10Inuka, nenda zako! 2 Kwa maana hapa sio mahali pako pa kupumzikia, 1 kwa sababu pametiwa unajisi, 2 pameharibiwa, wala hapatengenezeki tena. 1
11Ikiwa mwongo na mdanganyifu atakuja na kusema, 2 ‘Nitawatabiria divai na pombe kwa wingi,’ 1 angekuwa ndiye nabii 2 anayekubalika na watu hawa! 1 Ahadi Ya Ukombozi 1
12“Hakika nitawakusanya ninyi nyote, ee Yakobo, 2 Hakika nitawaleta pamoja mabaki ya Israeli. 1 Nitawaleta pamoja kama kondoo ndani ya zizi, 2 kama kundi kwenye malisho yake, 2 mahali hapa patakuwa na msongamano wa watu. 1
13Yeye afunguaye njia atawatangulia; 2 watapita kwenye lango na kutoka nje. 1 Mfalme wao atawatangulia, 2 Bwana atakuwa kiongozi.”