Song of Solomon · Biblia (Kiswahili)

Song of Solomon 2

1Mimi ni ua la Sharoni, 2 yungiyungi ya bondeni. Mpenzi 1

2Kama yungiyungi katikati ya miiba 2 ndivyo alivyo mpenzi wangu katikati ya wanawali. Mpendwa 1

3Kama mti wa mtofaa miongoni mwa miti ya msituni 2 ndivyo alivyo mpenzi wangu 2 miongoni mwa wanaume vijana. 1 Ninafurahia kuketi kivulini mwa mwanaume huyu, 2 na tunda lake ni tamu kwangu. 1

4Amenichukua mpaka kwenye ukumbi wa karamu, 2 na bendera ya huyu mwanaume 2 juu yangu ni upendo. 1

5Nitie nguvu kwa zabibu kavu, 2 niburudishe kwa matofaa, 2 kwa maana ninazimia kwa mapenzi. 1

6Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu, 2 na mkono wake wa kuume unanikumbatia. 1

7Binti za Yerusalemu, ninawaagiza 2 kwa paa na kwa ayala wa shambani: 1 Msichochee wala kuamsha mapenzi 2 hata yatakapotaka yenyewe. 1 Shairi La Pili Mpendwa 1

8Sikiliza! Mpenzi wangu! 2 Tazama! Huyu hapa anakuja, 1 akirukaruka juu milimani 2 akizunguka juu ya vilima. 1

9Mpenzi wangu ni kama paa au ayala kijana. 2 Tazama! Anasimama nyuma ya ukuta wetu, 1 akitazama kupitia madirishani, 2 akichungulia kimiani. 1

10Mpenzi wangu alizungumza na kuniambia, 2 “Inuka, mpenzi wangu, 2 mrembo wangu, tufuatane. 1

11Tazama! Wakati wa masika umepita, 2 mvua imekwisha na ikapita. 1

12Maua yanatokea juu ya nchi; 2 majira ya kuimba yamewadia, 1 sauti za njiwa zinasikika 2 katika nchi yetu. 1

13Mtini unatunga matunda yake ya mwanzoni, 2 zabibu zinazochanua zaeneza harufu nzuri. 1 Inuka, njoo mpenzi wangu. 2 Mrembo wangu, tufuatane.” Mpenzi 1

14Hua wangu penye nyufa za majabali, 2 mafichoni pembezoni mwa mlima, 1 nionyeshe uso wako, 2 na niisikie sauti yako, 1 kwa maana sauti yako ni tamu, 2 na uso wako unapendeza. 1

15Tukamatie mbweha, 2 mbweha wale wadogo 1 wanaoharibu mashamba ya mizabibu, 2 mashamba yetu ya mizabibu yaliyochanua. Mpendwa 1

16Mpenzi wangu ni wangu, nami ni wake, 2 yeye hujilisha katikati ya yungiyungi. 1

17Mpaka jua linapochomoza, 2 na vivuli vikimbie, 1 rudi, mpenzi wangu, 2 na uwe kama paa, 1 au kama ayala kijana 2 juu ya vilima vya Betheri.

← Song of Solomon 1Read In The App, Free →Song of Solomon 3 →

Study Song of Solomon 2

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

12345678