Hosea 12
1Efraimu anajilisha upepo; 2 hufukuzia upepo wa mashariki kutwa nzima 2 na kuzidisha uongo na jeuri. 1 Anafanya mkataba na Ashuru 2 na kutuma mafuta ya zeituni Misri. 1
2Bwana analo shtaka dhidi ya Yuda, 2 atamwadhibu Yakobo kwa kadiri ya njia zake 2 na kumlipa kwa kadiri ya matendo yake. 1
3Yakobo akiwa tumboni alishika kisigino cha kaka yake; 2 kama mwanadamu, alishindana na Mungu. 1
4Alishindana na malaika na kumshinda; 2 alilia na kuomba upendeleo wake. 1 Alimkuta huko Betheli 2 na kuzungumza naye huko: 1
5Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, 2 Bwana ndilo jina lake! 1
6Lakini ni lazima urudi kwa Mungu wako; 2 dumisha upendo na haki, 2 nawe umngojee Mungu wako siku zote. 1
7Mfanyabiashara hutumia vipimo vya udanganyifu; 2 hupenda kupunja. 1
8Efraimu hujisifu akisema, 2 “Mimi ni tajiri sana; nimetajirika. 1 Pamoja na utajiri wangu wote hawatakuta ndani yangu 2 uovu wowote au dhambi.” 1
9“Mimi ndimi Bwana Mungu wenu 2 niliyewaleta kutoka Misri; 1 nitawafanya mkae tena kwenye mahema, 2 kama vile katika siku 2 za sikukuu zenu zilizoamriwa. 1
10Niliongea na manabii, nikawapa maono mengi 2 na kusema mifano kupitia wao.” 1
11Je, Gileadi si mwovu? 2 Watu wake hawafai kitu! 1 Je, hawatoi dhabihu za mafahali huko Gilgali? 2 Madhabahu zao zitakuwa 2 kama malundo ya mawe 2 katika shamba lililolimwa. 1
12Yakobo alikimbilia katika nchi ya Aramu; 2 Israeli alitumika ili apate mke, 2 ili aweze kulipa kwa ajili yake alichunga kondoo. 1
13Bwana alimtumia nabii 2 kumpandisha Israeli kutoka Misri, 2 kwa njia ya nabii alimtunza. 1
14Lakini Efraimu amemchochea sana hasira; 2 Bwana wake ataleta juu yake 1 hatia yake ya kumwaga damu naye atamlipiza 2 kwa ajili ya dharau yake.