Hosea 8
1“Wekeni tarumbeta midomoni mwenu! 2 Tai yuko juu ya nyumba ya Bwana 1 kwa sababu watu wamevunja Agano langu, 2 wameasi dhidi ya sheria yangu. 1
2Israeli ananililia, 2 ‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’ 1
3Lakini Israeli amekataa lile lililo jema, 2 adui atamfuatia. 1
4Wanaweka wafalme bila idhini yangu, 2 wamechagua wakuu bila kibali changu. 1 Kwa fedha zao na dhahabu 2 wamejitengenezea sanamu kwa ajili 2 ya maangamizi yao wenyewe. 1
5Ee Samaria, tupilieni mbali sanamu yenu ya ndama! 2 Hasira yangu inawaka dhidi yao. 1 Watakuwa najisi mpaka lini? 2
6Zimetoka katika Israeli! 1 Ndama huyu: ametengenezwa na fundi, si Mungu. 2 Atavunjwa vipande vipande, 2 yule ndama wa Samaria. 1
7“Wanapanda upepo 2 na kuvuna upepo wa kisulisuli. 1 Bua halina suke, 2 halitatoa unga. 1 Kama lingetoa nafaka, 2 wageni wangeila yote. 1
8Israeli amemezwa; 2 sasa yupo miongoni mwa mataifa 2 kama kitu kisicho na thamani. 1
9Kwa kuwa wamepanda kwenda Ashuru 2 kama punda-mwitu anayetangatanga peke yake. 1 Efraimu amejiuza mwenyewe 2 kwa wapenzi. 1
10Ingawa wamejiuza wenyewe miongoni mwa mataifa, 2 sasa nitawakusanya pamoja. 1 Wataanza kudhoofika chini ya uonevu 2 wa mfalme mwenye nguvu. 1
11“Ingawa Efraimu alijenga madhabahu nyingi 2 kwa ajili ya sadaka za dhambi, 1 hizi zimekuwa madhabahu 2 za kufanyia dhambi. 1
12Nimeandika kwa ajili yao mambo mengi 2 kuhusu sheria yangu, 1 lakini wameziangalia 2 kama kitu cha kigeni. 1
13Wanatoa dhabihu nilizopewa mimi 2 nao wanakula hiyo nyama, 2 lakini Bwana hapendezwi nao. 1 Sasa ataukumbuka uovu wao 2 na kuadhibu dhambi zao: 2 Watarudi Misri. 1
14Israeli amemsahau Muumba wake 2 na kujenga majumba ya kifalme, 2 Yuda amejengea miji mingi ngome. 1 Lakini nitatuma moto kwenye miji yao 2 utakaoteketeza ngome zao.”