Proverbs 11
1Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, 2 bali vipimo sahihi ni furaha yake. 1
2Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, 2 bali unyenyekevu huja na hekima. 1
3Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, 2 bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao. 1
4Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, 2 bali haki huokoa kutoka mautini. 1
5Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, 2 bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe. 1
6Haki ya wanyofu huwaokoa, 2 bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya. 1
7Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; 2 yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu. 1
8Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, 2 naye mtu mwovu huingia humo badala yake. 1
9Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu 2 humwangamiza jirani yake, 2 bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa. 1
10Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; 2 mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha. 1
11Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, 2 bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa. 1
12Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, 2 bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake. 1
13Masengenyo husaliti tumaini, 2 bali mtu mwaminifu hutunza siri. 1
14Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, 2 bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika. 1
15Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, 2 bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama. 1
16Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, 2 bali wanaume wakorofi hupata mali tu. 1
17Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, 2 bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe. 1
18Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, 2 bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika. 1
19Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, 2 bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake. 1
20Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, 2 bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama. 1
21Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, 2 bali wenye haki watakuwa huru. 1
22Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe 2 ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara. 1
23Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, 2 bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu. 1
24Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, 2 mwingine huzuia, lakini huwa maskini. 1
25Mtu mkarimu atastawi; 2 yeye awaburudishaye wengine 2 ataburudishwa mwenyewe. 1
26Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, 2 bali baraka itamkalia kichwani kama taji 2 yeye aliye radhi kuiuza. 1
27Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, 2 bali ubaya huja kwake yeye autafutaye. 1
28Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, 2 bali mwenye haki atastawi kama jani bichi. 1
29Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, 2 naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima. 1
30Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, 2 naye mwenye hekima huvuta roho za watu. 1
31Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, 2 si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?