Proverbs · Biblia (Kiswahili)

Proverbs 31

1Misemo ya Mfalme Lemueli, usia wa mama yake aliyomfundisha: 1

2“Ee mwanangu, ee mwana wa tumbo langu, 2 ee mwana wa nadhiri zangu, + 31:2 Au: Ewe uliye jibu la maombi yangu. 1

3Usitumie nguvu zako kwa wanawake, 2 uhodari wako kwa wale wanaowaharibu wafalme. 1

4“Ee Lemueli, haifai wafalme, 2 haifai wafalme kunywa mvinyo, 2 haifai watawala kutamani sana kileo, 1

5wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru 2 na kuwanyima haki zao wote walioonewa. 1

6Wape kileo wale wanaoangamia, 2 mvinyo wale walio na uchungu, 1

7Wanywe na kusahau umaskini wao 2 na wasikumbuke taabu yao tena. 1

8“Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea, 2 kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa. 1

9Sema na uamue kwa haki, 2 tetea haki za maskini na wahitaji.” 1 Maneno Ya Mwisho: Mke Mwenye Sifa Nzuri 1

10Mke mwenye sifa nzuri, ni nani awezaye kumpata? 2 Yeye ni wa thamani sana kuliko marijani. + 31:10 Mithali 31:10-31 imetungwa kila mstari ukianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22. 1

11Mume wake anamwamini kikamilifu 2 wala hakosi kitu chochote cha thamani. 1

12Humtendea mumewe mema, wala si mabaya, 2 siku zote za maisha yake. 1

13Huchagua sufu na kitani 2 naye hufanya kazi kwa mikono yenye bidii. 1

14Yeye ni kama meli za biashara 2 akileta chakula chake kutoka mbali. 1

15Yeye huamka kungali bado giza 2 huwapa jamaa yake chakula 2 na mafungu kwa watumishi wake wa kike. 1

16Huangalia shamba na kulinunua, 2 kutokana na mapato yake hupanda shamba la mizabibu. 1

17Hufanya kazi zake kwa nguvu, 2 mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake. 1

18Huona kwamba biashara yake ina faida, 2 wala taa yake haizimiki usiku. 1

19Huweka mikono yake kwenye pia, 2 navyo vidole vyake hushikilia kijiti chenye uzi. 1

20Huwanyooshea maskini mikono yake 2 na kuwakunjulia wahitaji vitanga vyake. 1

21Theluji ishukapo, hana hofu kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, 2 kwa maana wote wamevikwa nguo za kutia joto. 1

22Hutengeneza mazulia ya urembo ya kufunika kitanda chake, 2 yeye huvaa kitani safi na urujuani. 1

23Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji, 2 aketipo miongoni mwa wazee wa nchi. 1

24Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, 2 naye huwauzia wafanyabiashara mishipi. 1

25Amevikwa nguvu na heshima, 2 anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo. 1

26Huzungumza kwa hekima 2 na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini mwake. 1

27Huangalia mambo ya nyumbani mwake 2 wala hali chakula cha uvivu. 1

28Watoto wake huamka na kumwita aliyebarikiwa, 2 mumewe pia humsifu, akisema: 1

29“Wanawake wengi hufanya vitu vyenye sifa nzuri, 2 lakini wewe umewapita wote.” 1

30Kujipamba ili kuvutia ni udanganyifu na uzuri unapita upesi, 2 bali mwanamke anayemcha Bwana atasifiwa. 1

31Mpe thawabu anayostahili, 2 nazo kazi zake na zimletee sifa kwenye lango la mji.

← Proverbs 30Read In The App, Free →Ecclesiastes 1 →

Study Proverbs 31

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

12345678910111213141516171819202122232425262728293031