Proverbs 23
1Uketipo kula chakula na mtawala, 2 angalia vyema kile kilicho mbele yako, 1
2na utie kisu kooni mwako 2 kama ukiwa mlafi. 1
3Usitamani vyakula vyake vitamu 2 kwa kuwa chakula hicho ni cha hila. 1
4Usijitaabishe ili kuupata utajiri, 2 uwe na hekima kuonyesha kujizuia. 1
5Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka, 2 huwa kama umepata mabawa ghafula, 2 ukaruka na kutoweka angani kama tai. 1
6Usile chakula cha mtu mchoyo, 2 usitamani vyakula vyake vitamu, 1
7kwa maana yeye ni aina ya mtu 2 ambaye kila mara anafikiri juu ya gharama. 1 Anakuambia, “Kula na kunywa,” 2 lakini moyo wake hauko pamoja nawe. 1
8Utatapika kile kidogo ulichokula, 2 nawe utakuwa umepoteza bure 2 maneno yako ya kumsifu. 1
9Usizungumze na mpumbavu, 2 kwa maana atadhihaki hekima ya maneno yako. 1
10Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani 2 wala kunyemelea kwenye mashamba ya yatima, 1
11kwa kuwa Mtetezi wao ni mwenye nguvu, 2 atalichukua shauri lao dhidi yako. 1
12Elekeza moyo wako kwenye mafundisho 2 na masikio yako kwenye maneno ya maarifa. 1
13Usimnyime mtoto adhabu, 2 ukimwadhibu kwa fimbo, hatakufa. 1
14Mwadhibu kwa fimbo 2 na kuiokoa nafsi yake kutoka mautini. + 23:14 Mautini maana yake ni Kuzimu. 1
15Mwanangu, kama moyo wako una hekima, 2 basi moyo wangu utafurahi, 1
16utu wangu wa ndani utafurahi, 2 wakati midomo yako 2 itakapozungumza lililo sawa. 1
17Usiuruhusu moyo wako kuwaonea wivu wenye dhambi, 2 bali kila mara uwe na bidii katika kumcha Bwana. 1
18Hakika kuna tumaini la baadaye kwa ajili yako, 2 nalo tarajio lako halitakatiliwa mbali. 1
19Sikiliza, mwanangu na uwe na hekima, 2 weka moyo wako kwenye njia iliyo sawa. 1
20Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo, 2 au wale walao nyama kwa pupa, 1
21kwa maana walevi na walafi huwa maskini, 2 nako kusinzia huwavika matambara. 1
22Msikilize baba yako, aliyekuzaa, 2 wala usimdharau mama yako atakapokuwa mzee. 1
23Nunua kweli wala usiiuze, 2 pata hekima, adabu na ufahamu. 1
24Baba wa mwenye haki ana furaha kubwa, 2 naye aliye na mwana mwenye hekima humfurahia. 1
25Baba yako na mama yako na wafurahi, 2 mama aliyekuzaa na ashangilie! 1
26Mwanangu, nipe moyo wako, 2 macho yako na yafuate njia zangu, 1
27kwa maana kahaba ni shimo refu 2 na mwanamke mpotovu ni kisima chembamba. 1
28Kama mnyangʼanyi, hungojea akivizia, 2 naye huzidisha wasio waaminifu miongoni mwa wanaume. 1
29Ni nani mwenye ole? 2 Ni nani mwenye huzuni? 1 Ni nani mwenye ugomvi? 2 Ni nani mwenye malalamiko? 1 Ni nani aliye na majeraha yasiyo na sababu? 2 Ni nani mwenye macho mekundu? 1
30Ni hao wakaao sana kwenye mvinyo, 2 hao waendao kuonja mabakuli ya mvinyo uliochanganywa. 1
31Usiukodolee macho mvinyo wakati ukiwa mwekundu, 2 wakati unapometameta kwenye bilauri, 2 wakati ushukapo taratibu! 1
32Mwishowe huuma kama nyoka 2 na kutia sumu yake kama nyoka mwenye sumu. 1
33Macho yako yataona mambo mageni 2 na moyo wako kuwazia mambo yaliyopotoka. 1
34Utakuwa kama alalaye katikati ya bahari, 2 alalaye juu ya kamba ya merikebu. 1
35Utasema, “Wamenipiga lakini sikuumia! 2 Wamenichapa, lakini sisikii! 1 Nitaamka lini 2 ili nikanywe tena?”