Proverbs 6
1Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, 2 ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi 2 kwa ajili ya mwingine, 1
2kama umetegwa na ulichosema, 2 umenaswa kwa maneno ya kinywa chako, 1
3basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, 2 kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: 1 Nenda ukajinyenyekeshe kwake; 2 msihi jirani yako! 1
4Usiruhusu usingizi machoni pako, 2 usiruhusu kope zako zisinzie. 1
5Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, 2 kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji. 1
6Ewe mvivu, mwendee mchwa; 2 zitafakari njia zake ukapate hekima! 1
7Kwa maana yeye hana msimamizi, 2 wala mwangalizi, au mtawala, 1
8lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi 2 na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno. 1
9Ewe mvivu, utalala hata lini? 2 Utaamka lini kutoka usingizi wako? 1
10Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, 2 bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika: 1
11hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, 2 na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha. 1
12Mtu mbaya sana na mlaghai, 2 ambaye huzungukazunguka 3 na maneno ya upotovu, 2
13ambaye anakonyeza kwa jicho lake, 2 anayetoa ishara kwa miguu yake 2 na kuashiria kwa vidole vyake, 2
14ambaye hupanga ubaya 3 kwa udanganyifu moyoni mwake: 2 daima huchochea fitina. 1
15Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; 2 ataangamizwa mara, pasipo msaada. 1
16Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, 2 naam, viko saba vilivyo chukizo kwake: 3
17macho ya kiburi, 3 ulimi udanganyao, 3 mikono imwagayo damu isiyo na hatia, 3
18moyo uwazao mipango miovu, 3 miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu, 3
19shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, 3 na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu. 1 Onyo Dhidi Ya Uasherati 1
20Mwanangu, zishike amri za baba yako, 2 wala usiyaache mafundisho ya mama yako. 1
21Yafunge katika moyo wako daima, 2 yakaze kuizunguka shingo yako. 1
22Wakati utembeapo, yatakuongoza; 2 wakati ulalapo, yatakulinda; 2 wakati uamkapo, yatazungumza nawe. 1
23Kwa maana amri hizi ni taa, 2 mafundisho haya ni mwanga 2 na maonyo ya maadili ni njia ya uzima, 1
24yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, 2 kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka. 1
25Moyo wako usitamani uzuri wake 2 wala macho yake yasikuteke, 1
26kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, 2 hata ukose kipande cha mkate, 2 naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa. 1
27Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake 2 bila nguo zake kuungua? 1
28Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka 2 bila miguu yake kuungua? 1
29Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; 2 hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa. 1
30Watu hawamdharau mwizi kama akiiba 2 kukidhi njaa yake wakati ana njaa. 1
31Pamoja na hayo, kama akikamatwa, 2 lazima alipe mara saba, 2 ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake. 1
32Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; 2 yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe. 1
33Mapigo na aibu ni fungu lake 2 na aibu yake haitafutika kamwe; 1
34kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, 2 naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi. 1
35Hatakubali fidia yoyote; 2 atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.