Proverbs 28
1Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, 2 bali wenye haki ni wajasiri kama simba. 1
2Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, 2 bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu. 1
3Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi 2 ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao. 1
4Wale waiachao sheria huwasifu waovu, 2 bali wale waishikao sheria huwapinga. 1
5Watu wabaya hawaelewi haki, 2 bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu. 1
6Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama 2 kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu. 1
7Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, 2 bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake. 1
8Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno 2 hukusanya kwa ajili ya mwingine, 2 ambaye atawahurumia maskini. 1
9Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, 2 hata maombi yake ni chukizo. 1
10Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, 2 ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, 2 bali wasio na lawama watapokea urithi mwema. 1
11Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, 2 bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua. 1
12Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, 2 bali waovu watawalapo, watu hujificha. 1
13Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, 2 bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema. 1
14Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, 2 bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu 2 huangukia kwenye taabu. 1
15Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, 2 ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge. 1
16Mtawala dhalimu hana akili, 2 bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu 2 atafurahia maisha marefu. 1
17Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua 2 atakuwa mtoro mpaka kufa; 2 mtu yeyote na asimsaidie. 1
18Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama 2 hulindwa salama, 1 bali yeye ambaye njia zake ni potovu 2 ataanguka ghafula. 1
19Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, 2 bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha. 1
20Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, 2 bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka 2 hataacha kuadhibiwa. 1
21Kuonyesha upendeleo si vizuri, 2 hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate. 1
22Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, 2 naye hana habari kuwa umaskini unamngojea. 1
23Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, 2 kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili. 1
24Yeye amwibiaye babaye au mamaye 2 na kusema, “Si kosa,” 2 yeye ni mwenzi wa yule aharibuye. 1
25Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, 2 bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa. 1
26Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, 2 bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama. 1
27Yeye ampaye maskini 2 hatapungukiwa na kitu chochote, 1 bali yeye awafumbiaye maskini macho 2 hupata laana nyingi. 1
28Wakati waovu watawalapo, 2 watu huenda mafichoni, 1 bali waovu wanapoangamia, 2 wenye haki hufanikiwa.