Proverbs · Biblia (Kiswahili)

Proverbs 13

1Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya babaye, 2 bali mwenye dharau hasikilizi maonyo. 1

2Kutoka tunda la midomo yake mtu hufurahia mambo mema, 2 bali wasio waaminifu wanatamani sana jeuri. 1

3Yeye alindaye midomo yake hulinda nafsi yake, 2 bali yeye asemaye kwa haraka ataangamia. 1

4Mvivu hutamani sana na hapati kitu, 2 bali nafsi ya mwenye bidii 2 hutoshelezwa kikamilifu. 1

5Mwenye haki huchukia uongo, 2 bali waovu huleta aibu na fedheha. 1

6Haki humlinda mtu mwadilifu, 2 bali uovu humwangusha mwenye dhambi. 1

7Mtu mmoja hujifanya tajiri, kumbe hana chochote; 1 mwingine hujifanya maskini, kumbe ana utajiri mwingi. 1

8Utajiri wa mtu waweza kukomboa maisha yake, 2 bali mtu maskini hasikii kitisho. 1

9Nuru ya mwenye haki hungʼaa sana, 2 bali taa ya mwovu itazimwa. 1

10Kiburi huzalisha magomvi tu, 2 bali hekima hupatikana kwa wale wanaozingatia ushauri. 1

11Fedha isiyo ya halali hupungua, 2 bali yeye akusanyaye fedha kidogo kidogo huongezeka. 1

12Kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua, 2 bali tumaini lililotimizwa ni mti wa uzima. 1

13Yeye anayedharau mafundisho anajiletea maangamizi, 2 bali yeye anayeheshimu agizo hupewa tuzo. 1

14Mafundisho ya mwenye busara ni chemchemi ya uzima, 2 ili kumwepusha mtu na mitego ya mauti. 1

15Ufahamu mzuri hupata upendeleo, 2 bali njia ya asiye mwaminifu ni ngumu. 1

16Kila mwenye busara hutenda kwa maarifa, 2 bali mpumbavu hudhihirisha upumbavu wake. 1

17Mjumbe mwovu huanguka kwenye taabu, 2 bali mjumbe mwaminifu huleta uponyaji. 1

18Yeye anayedharau maonyo hupata umaskini na aibu, 2 bali yeye anayekubali maonyo huheshimiwa. 1

19Tarajio lililotimizwa ni tamu kwa nafsi, 2 bali wapumbavu huchukia sana kuacha ubaya. 1

20Yeye atembeaye na mwenye hekima atapata hekima, 2 bali rafiki wa mpumbavu hupata madhara. 1

21Balaa humwandama mtenda dhambi, 2 bali mafanikio ni thawabu kwa mwenye haki. 1

22Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi, 2 bali mali ya wenye dhambi imehifadhiwa 2 kwa ajili ya wenye haki. 1

23Shamba la mtu maskini laweza kuzalisha chakula kingi, 2 bali dhuluma hukifutilia mbali. 1

24Yeye aizuiaye fimbo yake hampendi mwanawe, 2 bali yeye ampendaye 2 huwa mwangalifu kumwadibisha. 1

25Mwenye haki hula mpaka akaridhisha moyo wake, 2 bali tumbo la mwovu hutaabika kwa njaa.

← Proverbs 12Read In The App, Free →Proverbs 14 →

Study Proverbs 13

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

12345678910111213141516171819202122232425262728293031