Proverbs · Biblia (Kiswahili)

Proverbs 26

1Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, 2 ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu. 1

2Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake 2 au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, 2 ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu. 1

3Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, 2 nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu! 1

4Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, 2 ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye. 1

5Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, 2 ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe. 1

6Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, 2 ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu. 1

7Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia 2 ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu. 1

8Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, 2 ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima. 1

9Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi 2 ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu. 1

10Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, 2 ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani. 1

11Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, 2 ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake. 1

12Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima 2 machoni pake mwenyewe? 2 Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake. 1

13Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, 2 simba mkali anazunguka mitaa!” 1

14Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, 2 ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake. 1

15Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, 2 naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake. 1

16Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, 2 kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara. 1

17Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, 2 ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu. 1

18Kama mtu mwendawazimu 2 atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha, 1

19ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, 2 “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!” 1

20Bila kuni moto huzimika; 2 pasipo uchongezi ugomvi humalizika. 1

21Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, 2 ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi. 1

22Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; 2 huingia sehemu za ndani sana za mtu. 1

23Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo 2 ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya. 1

24Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, 2 lakini moyoni mwake huficha udanganyifu. 1

25Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, 2 kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake. 1

26Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, 2 lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko. 1

27Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, 2 kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia. 1

28Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, 2 nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

← Proverbs 25Read In The App, Free →Proverbs 27 →

Study Proverbs 26

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

12345678910111213141516171819202122232425262728293031