Proverbs · Biblia (Kiswahili)

Proverbs 27

1Usijisifu kwa ajili ya kesho, 2 kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja. 1

2Mwache mwingine akusifu, 2 wala si kinywa chako mwenyewe; 1 mtu mwingine afanye hivyo 2 na si midomo yako mwenyewe. 1

3Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, 2 lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili. 1

4Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, 2 lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu? 1

5Afadhali karipio la wazi 2 kuliko upendo uliofichika. 1

6Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, 2 bali kubusu kwa adui ni kwingi sana. 1

7Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, 2 bali kwa mwenye njaa 2 hata kile kilicho kichungu 2 kwake ni kitamu. 1

8Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, 2 ndivyo alivyo mtu atangatangaye 2 mbali na nyumbani mwake. 1

9Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, 2 nao uzuri wa rafiki huchipuka 2 kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu. 1

10Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, 2 tena usiende nyumbani mwa ndugu yako 2 wakati umepatwa na maafa. 1 Bora jirani wa karibu 2 kuliko ndugu aliye mbali. 1

11Mwanangu, uwe na hekima, 2 nawe ulete furaha moyoni mwangu, 1 ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote 2 anitendaye kwa dharau. 1

12Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, 2 bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa. 1

13Chukua vazi la yule awekaye dhamana 2 kwa ajili ya mgeni; 1 lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo 2 kwa ajili ya mwanamke mpotovu. 1

14Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu 2 asubuhi na mapema, 2 itahesabiwa kama ni laana. 1

15Mke mgomvi ni kama 2 matone yasiyokoma ya siku ya mvua. 1

16Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo 2 au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono. 1

17Kama vile chuma kinoavyo chuma, 2 ndivyo mtu amnoavyo mwenzake. 1

18Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, 2 naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa. 1

19Kama uso uonekanavyo kwenye maji, 2 ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo. 1

20Kuzimu na Uharibifu havishibi 2 kadhalika macho ya mwanadamu. 1

21Kalibu ni kwa ajili ya fedha 2 na tanuru kwa ajili ya dhahabu, 2 bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo. 1

22Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, 2 ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, 2 hutauondoa upumbavu wake. 1

23Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako 2 ya kondoo na mbuzi, 2 angalia kwa bidii ngʼombe zako. 1

24Kwa kuwa utajiri haudumu milele, 2 nayo taji haidumu vizazi vyote. 1

25Wakati majani makavu yameondolewa 2 na mapya yamechipua, 2 nayo majani toka milimani yamekusanywa, 1

26wana-kondoo watakupatia mavazi 2 na mbuzi thamani ya shamba. 1

27Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi 2 kukulisha wewe na jamaa yako, 2 na kuwalisha watumishi wako wa kike.

← Proverbs 26Read In The App, Free →Proverbs 28 →

Study Proverbs 27

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

12345678910111213141516171819202122232425262728293031