Proverbs · Biblia (Kiswahili)

Proverbs 8

1Je, hekima haitani? 2 Je, ufahamu hapazi sauti? 1

2Juu ya miinuko karibu na njia, 2 penye njia panda, ndipo asimamapo; 1

3kando ya malango yaelekeayo mjini, 2 kwenye maingilio, hulia kwa sauti kubwa, akisema: 1

4“Ni ninyi wanaume, ninaowaita; 2 ninapaza sauti yangu kwa wanadamu wote. 1

5Ninyi ambao ni wajinga, pateni akili; 2 ninyi mlio wapumbavu, pateni ufahamu. 1

6Sikilizeni, kwa maana nina mambo muhimu ya kusema; 2 ninafungua midomo yangu kusema lililo sawa. 1

7Kinywa changu husema lililo kweli, 2 kwa maana midomo yangu huchukia uovu. 1

8Maneno yote ya kinywa changu ni haki; 2 hakuna mojawapo lililopotoka wala ukaidi. 1

9Kwa wenye kupambanua yote ni sahihi; 2 hayana kasoro kwa wale wenye maarifa. 1

10Chagua mafundisho yangu badala ya fedha, 2 maarifa badala ya dhahabu safi, 1

11kwa maana hekima ina thamani kuliko marijani 2 na hakuna chochote unachohitaji kinacholingana naye. 1

12“Mimi hekima, nakaa pamoja na busara; 2 ninamiliki maarifa na busara. 1

13Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; 2 ninachukia kiburi na majivuno, 2 tabia mbaya na mazungumzo potovu. 1

14Ushauri na hukumu sahihi ni vyangu; 2 nina ufahamu na nina nguvu. 1

15Kwa msaada wangu wafalme hutawala 2 na watawala hutunga sheria zilizo za haki, 1

16kwa msaada wangu wakuu hutawala, 2 na wenye vyeo wote watawalao dunia. 1

17Nawapenda wale wanipendao, 2 na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. 1

18Utajiri na heshima viko kwangu, 2 utajiri udumuo na mafanikio. 1

19Tunda langu ni bora kuliko dhahabu safi; 2 kile nitoacho hupita fedha iliyo bora. 1

20Natembea katika njia ya unyofu 2 katika mapito ya haki, 1

21nawapa utajiri wale wanipendao 2 na kuzijaza hazina zao. 1

22“ Bwana aliniumba mwanzoni mwa kazi yake, 2 kabla ya matendo yake ya zamani; 1

23niliteuliwa tangu milele, 2 tangu mwanzoni, kabla ya dunia kuumbwa. 1

24Wakati hazijakuwepo bahari, nilikwishazaliwa, 2 wakati hazijakuwepo chemchemi zilizojaa maji; 1

25kabla milima haijawekwa mahali pake, 2 kabla vilima havijakuwepo, nilikwishazaliwa, 1

26kabla hajaumba dunia wala mashamba yake 2 au vumbi lolote la dunia. 1

27Nilikuwepo alipoziweka mbingu mahali pake, 2 wakati alichora mstari wa upeo wa macho 3 juu ya uso wa kilindi, 1

28wakati aliweka mawingu juu 2 na kuziweka imara chemchemi za bahari, 1

29wakati aliiwekea bahari mpaka wake 2 ili maji yasivunje agizo lake, 1 na wakati aliweka misingi ya dunia. 2

30Wakati huo nilikuwa fundi stadi kando yake. 1 Nilijazwa na furaha siku baada ya siku, 2 nikifurahi daima mbele zake, 1

31nikifurahi katika dunia yake yote 2 nami nikiwafurahia wanadamu. 1

32“Basi sasa wanangu, nisikilizeni; 2 heri wale wanaozishika njia zangu. 1

33Sikilizeni mafundisho yangu mwe na hekima; 2 msiyapuuze. 1

34Heri mtu yule anisikilizaye mimi, 2 akisubiri siku zote malangoni mwangu, 2 akingoja kwenye vizingiti vya mlango wangu. 1

35Kwa maana yeyote anipataye mimi amepata uzima 2 na kujipatia kibali kutoka kwa Bwana. 1

36Lakini yeyote ashindwaye kunipata 2 hujiumiza mwenyewe; 2 na wote wanichukiao mimi hupenda mauti.”

← Proverbs 7Read In The App, Free →Proverbs 9 →

Study Proverbs 8

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

12345678910111213141516171819202122232425262728293031