Proverbs · Biblia (Kiswahili)

Proverbs 15

1Jawabu la upole hugeuza ghadhabu, 2 bali neno liumizalo huchochea hasira. 1

2Ulimi wa mwenye hekima husifu maarifa, 2 bali kinywa cha mpumbavu hufoka upumbavu. 1

3Macho ya Bwana yako kila mahali, 2 yakiwaangalia waovu na wema. 1

4Ulimi uletao uponyaji ni mti wa uzima, 2 bali ulimi udanganyao huponda roho. 1

5Mpumbavu hubeza maonyo ya baba yake, 2 bali yeyote akubaliye maonyo huonyesha busara. 1

6Nyumba ya mwenye haki ina hazina kubwa, 2 bali mapato ya waovu huwaletea taabu. 1

7Midomo ya mwenye hekima hueneza maarifa, 2 bali sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu. 1

8Bwana huchukia sana dhabihu za waovu, 2 bali maombi ya wanyofu humfurahisha Mungu. 1

9Bwana huchukia sana njia ya waovu, 2 bali huwapenda wale wafuatao haki. 1

10Adhabu kali humngoja yeye aachaye njia; 2 yeye achukiaye maonyo atakufa. 1

11Mauti + 15:11 Yaani Sheol, maana yake ni Kuzimu. na Uharibifu + 15:11 Kwa Kiebrania ni Abadon. viko wazi mbele za Bwana: 2 je, si zaidi sana mioyo ya wanadamu! 1

12Mwenye mzaha huchukia maonyo; 2 hatataka shauri kwa mwenye hekima. 1

13Moyo wenye furaha hufanya uso uchangamke, 2 bali maumivu ya moyoni huponda roho. 1

14Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, 2 bali kinywa cha mpumbavu hujilisha upumbavu. 1

15Siku zote za wanaoonewa ni za taabu, 2 bali moyo mchangamfu una karamu ya kudumu. 1

16Afadhali kuwa na kidogo pamoja na kumcha Bwana, 2 kuliko mali nyingi pamoja na ghasia. 1

17Afadhali chakula cha mboga mahali palipo na upendo 2 kuliko nyama ya ndama iliyonona pamoja na chuki. 1

18Mtu mwepesi wa hasira huchochea ugomvi, 2 bali mtu mvumilivu hutuliza ugomvi. 1

19Njia ya mvivu imezibwa na miiba, 2 bali njia ya mwenye haki ni barabara kuu. 1

20Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, 2 bali mtu mpumbavu humdharau mama yake. 1

21Upumbavu humfurahisha mtu ambaye hana akili, 2 bali mtu mwenye ufahamu hushika njia iliyonyooka. 1

22Mipango hushindwa kufanikiwa kwa ajili ya kukosa ushauri, 2 bali kukiwa na washauri wengi hufanikiwa. 1

23Mtu hupata furaha katika kutoa jibu linalofaa: 2 je, ni zuri namna gani neno lililotoka kwa wakati wake! 1

24Mapito ya uzima huelekea juu kwa ajili ya wenye hekima 2 kumwepusha asiende chini kaburini. 1

25Bwana hubomoa nyumba ya mtu mwenye kiburi, 2 bali huilinda mipaka ya mjane isiguswe. 1

26Bwana huchukia sana mawazo ya mwovu, 2 bali mawazo ya wale walio safi humfurahisha yeye. 1

27Mtu mwenye tamaa huletea jamaa yake taabu, 2 bali yeye achukiaye rushwa ataishi. 1

28Moyo wa mwenye haki hupima majibu yake, 2 bali kinywa cha mwovu hufoka ubaya. 1

29Bwana yuko mbali na waovu, 2 bali husikia maombi ya wenye haki. 1

30Mtazamo wa tabasamu huleta furaha moyoni, 2 nazo habari njema huipa mifupa afya. 1

31Yeye asikilizaye maonyo yatoayo uzima 2 atakuwa miongoni mwa wenye hekima. 1

32Yeye anayedharau maonyo hujidharau mwenyewe, 2 bali yeyote anayekubali maonyo hupata ufahamu. 1

33Kumcha Bwana humfundisha mtu hekima, 2 nao unyenyekevu huja kabla ya heshima.

← Proverbs 14Read In The App, Free →Proverbs 16 →

Study Proverbs 15

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

12345678910111213141516171819202122232425262728293031