Proverbs · Biblia (Kiswahili)

Proverbs 7

1Mwanangu, shika maneno yangu 2 na kuzihifadhi amri zangu ndani yako. 1

2Shika amri zangu nawe utaishi; 2 linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako. 1

3Yafunge katika vidole vyako; 2 yaandike katika kibao cha moyo wako. 1

4Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” 2 uite ufahamu jamaa yako; 1

5watakuepusha na mwanamke mzinzi, 2 kutokana na mwanamke mpotovu 2 na maneno yake ya kubembeleza. 1

6Kwenye dirisha la nyumba yangu 2 nilitazama nje kupitia upenyo 2 kwenye mwimo wa dirisha. 1

7Niliona miongoni mwa wajinga, 2 nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, 2 kijana asiye na akili. 1

8Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, 2 akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke 1

9wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, 2 giza la usiku lilipokuwa likiingia. 1

10Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, 2 hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu. 1

11(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, 2 miguu yake haitulii nyumbani; 1

12mara kwenye barabara za mji, 2 mara kwenye viwanja vikubwa, 2 kwenye kila pembe huvizia.) 1

13Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, 2 na kwa uso usio na haya akamwambia: 1

14“Nina sadaka za amani nyumbani; 2 leo nimetimiza nadhiri zangu. 1

15Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; 2 nimekutafuta na nimekupata! 1

16Nimetandika kitanda changu 2 kwa kitani za rangi kutoka Misri. 1

17Nimetia manukato kitanda changu 2 kwa manemane, udi na mdalasini. 1

18Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; 2 tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi! 1

19Mume wangu hayupo nyumbani; 2 amekwenda safari ya mbali. 1

20Amechukua mkoba uliojazwa fedha 2 na hatakuwepo nyumbani karibuni.” 1

21Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; 2 alimshawishi kwa maneno yake laini. 1

22Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke 2 kama fahali aendaye machinjoni, 2 kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi, 1

23mpaka mshale umchome ini lake, 2 kama ndege anayenaswa kwenye mtego, 2 bila kujua itamgharimu maisha yake. 1

24Sasa basi wanangu, nisikilizeni; 2 sikilizeni kwa makini nisemalo. 1

25Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke, 2 wala usitangetange katika mapito yake. 1

26Aliowaangusha ni wengi; 2 aliowachinja ni kundi kubwa. 1

27Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, + 7:27 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. 2 ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti.

← Proverbs 6Read In The App, Free →Proverbs 8 →

Study Proverbs 7

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

12345678910111213141516171819202122232425262728293031