Proverbs 3
1Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, 2 bali zitunze amri zangu moyoni mwako, 1
2kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako 2 na kukuletea mafanikio. 1
3Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; 2 vifunge shingoni mwako, 2 viandike katika ubao wa moyo wako. 1
4Ndipo utapata kibali na jina zuri 2 mbele za Mungu na mwanadamu. 1
5Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote 2 wala usizitegemee akili zako mwenyewe; 1
6katika njia zako zote mkiri yeye, 2 naye atayanyoosha mapito yako. 1
7Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; 2 mche Bwana ukajiepushe na uovu. 1
8Hii itakuletea afya mwilini mwako, 2 na mafuta kwenye mifupa yako. 1
9Mheshimu Bwana kwa mali zako na 2 kwa malimbuko ya mazao yako yote; 1
10ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, 2 viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya. 1
11Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana 2 na usichukie kukaripiwa naye, 1
12kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, 2 kama vile baba afanyavyo 2 kwa mwana apendezwaye naye. 1
13Heri mtu yule aonaye hekima, 2 mtu yule apataye ufahamu, 1
14kwa maana hekima ana faida kuliko fedha 2 na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi. 1
15Hekima ana thamani kuliko marijani; 2 hakuna chochote unachokitamani 2 kinachoweza kulinganishwa naye. 1
16Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; 2 katika mkono wake wa kushoto 2 kuna utajiri na heshima. 1
17Njia zake zinapendeza, 2 mapito yake yote ni amani. 1
18Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; 2 wale wamshikao watabarikiwa. 1
19Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, 2 kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake; 1
20kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, 2 nayo mawingu yanadondosha umande. 1
21Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, 2 usiache vitoke machoni pako; 1
22ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako 2 na pambo la neema shingoni mwako. 1
23Kisha utaenda katika njia yako salama, 2 wala mguu wako hautajikwaa; 1
24ulalapo, hautaogopa; 2 ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu. 1
25Usiogope maafa ya ghafula 2 au maangamizi yanayowapata waovu, 1
26kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako 2 na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego. 1
27Usizuie wema kwa wale wanaostahili 2 ikiwa katika uwezo wako kutenda. 1
28Usimwambie jirani yako, 2 “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: 2 wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe. 1
29Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, 2 ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini. 1
30Usimshtaki mtu bila sababu, 2 wakati hajakutenda dhara lolote. 1
31Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri 2 wala kuchagua njia yake iwayo yote, 1
32kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, 2 lakini siri yake iko kwa mwenye haki. 1
33Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, 2 lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki. 1
34Huwadhihaki wale wanaodhihaki, 2 lakini huwapa neema wale wanyenyekevu. 1
35Wenye hekima hurithi heshima, 2 bali huwaaibisha wapumbavu.