Proverbs 16
1Mipango ya moyoni ni ya mwanadamu, 2 bali jibu la ulimi hutoka kwa Bwana. 1
2Njia zote za mtu huonekana safi machoni pake mwenyewe, 2 bali makusudi hupimwa na Bwana. 1
3Mkabidhi Bwana lolote ufanyalo, 2 nayo mipango yako itafanikiwa. 1
4Bwana hufanya kila kitu kwa kusudi lake mwenyewe; 2 hata waovu kwa siku ya maangamizi. 1
5Bwana huwachukia sana wote wenye kiburi cha moyo. 2 Uwe na hakika kwa hili: Hawataepuka kuadhibiwa. 1
6Kwa upendo na uaminifu uovu huondolewa; 2 kwa kumcha Bwana mtu hujiepusha na ubaya. 1
7Njia za mtu zinapompendeza Bwana, 2 huwafanya hata adui zake waishi naye kwa amani. 1
8Afadhali kitu kidogo pamoja na haki 2 kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu. 1
9Moyo wa mtu huifikiri njia yake, 2 bali Bwana huelekeza hatua zake. 1
10Midomo ya mfalme huzungumza kwa hekima ya kiungu, 2 wala kinywa chake hakipotoshi haki. 1
11Vipimo na mizani za halali hutoka kwa Bwana; 2 mawe yote ya kupimia yaliyo katika mfuko ameyafanya yeye. 1
12Wafalme huchukia sana kutenda maovu, 2 kwa maana kiti cha ufalme hufanywa imara kwa njia ya haki. 1
13Wafalme hufurahia midomo ya uaminifu; 2 humthamini mtu asemaye kweli. 1
14Ghadhabu ya mfalme ni mjumbe wa mauti, 2 bali mtu mwenye hekima ataituliza. 1
15Uso wa mfalme ungʼaapo, inamaanisha uhai; 2 upendeleo wake ni kama wingu la mvua wakati wa vuli. 1
16Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu, 2 kuchagua ufahamu kuliko fedha! 1
17Njia kuu ya wanyofu huepuka ubaya; 2 yeye aichungaye njia yake, huchunga maisha yake. 1
18Kiburi hutangulia maangamizi, 2 roho ya majivuno hutangulia maanguko. 1
19Ni afadhali kuwa mnyenyekevu katika roho 2 miongoni mwa walioonewa 2 kuliko kugawana nyara pamoja na wenye kiburi. 1
20Yeyote anayekubali mafundisho hustawi, 2 tena amebarikiwa yeye anayemtumaini Bwana. 1
21Wenye hekima moyoni huitwa wenye ufahamu, 2 na maneno ya kupendeza huchochea mafundisho. 1
22Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwa wale walio nao, 2 bali upumbavu huleta adhabu kwa wapumbavu. 1
23Moyo wa mtu mwenye hekima huongoza kinywa chake, 2 na midomo yake huchochea mafundisho. 1
24Maneno ya kupendeza ni kama sega la asali, 2 ni matamu kwa nafsi na uponyaji kwenye mifupa. 1
25Iko njia ionekanayo kuwa sawa kwa mtu, 2 bali mwisho wake huelekeza mautini. 1
26Shauku ya mfanyakazi humhimiza kufanya kazi; 2 njaa yake humsukuma aendelee. 1
27Mtu mbaya kabisa hupanga mabaya, 2 maneno yake ni kama moto uunguzao. 1
28Mtu mpotovu huchochea ugomvi, 2 nayo maongezi ya upuzi hutenganisha marafiki wa karibu. 1
29Mtu mkali humvuta jirani yake 2 na kumwongoza katika mapito yale mabaya. 1
30Yeye akonyezaye kwa jicho lake anapanga upotovu; 2 naye akazaye midomo yake amenuia mabaya. 1
31Mvi ni taji ya utukufu; 2 hupatikana kwa maisha ya uadilifu. 1
32Ni afadhali mtu mstahimilivu kuliko shujaa, 2 mtu anayeitawala hasira yake kuliko yule autekaye mji. 1
33Kura hupigwa kwa siri, 2 lakini kila uamuzi wake hutoka kwa Bwana.