Proverbs · Biblia (Kiswahili)

Proverbs 17

1Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu 2 kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi. 1

2Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, 2 naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu. 1

3Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, 2 bali Bwana huujaribu moyo. 1

4Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; 2 mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara. 1

5Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; 2 yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa. 1

6Wana wa wana ni taji la wazee, 2 nao wazazi ni fahari ya watoto wao. 1

7Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: 2 je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala! 1

8Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; 2 kokote kigeukiapo, hufanikiwa. 1

9Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, 2 bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu. 1

10Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua 2 kuliko mapigo mia kwa mpumbavu. 1

11Mtu mbaya hupenda kuasi tu; 2 mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake. 1

12Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, 2 kuliko mpumbavu katika upumbavu wake. 1

13Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, 2 kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake. 1

14Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; 2 kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza. 1

15Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, 2 naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: 2 Bwana huwachukia sana wote wawili. 1

16Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, 2 wakati yeye hana haja ya kupata hekima? 1

17Rafiki hupenda wakati wote 2 naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida. 1

18Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, 2 naye huweka dhamana kwa jirani yake. 1

19Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; 2 naye ainuaye sana lango lake + 17:19 Kuinua lango maana yake ni kusema kwa majivuno. hutafuta uharibifu. 1

20Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; 2 naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu. 1

21Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; 2 hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu. 1

22Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, 2 bali roho iliyopondeka hukausha mifupa. 1

23Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri 2 ili kupotosha njia ya haki. 1

24Mtu wa ufahamu huitazama hekima, 2 lakini macho ya mpumbavu huhangaika 2 hadi kwenye miisho ya dunia. 1

25Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake 2 na uchungu kwa yeye aliyemzaa. 1

26Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, 2 au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao. 1

27Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, 2 naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu. 1

28Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, 2 na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

← Proverbs 16Read In The App, Free →Proverbs 18 →

Study Proverbs 17

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

12345678910111213141516171819202122232425262728293031