Job 10
1“Nayachukia sana haya maisha yangu; 2 kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia, 2 nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu. 1
2Nitamwambia Mungu: Usinihukumu, 2 bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu. 1
3Je, inakupendeza wewe kunionea, 2 kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako, 2 huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu? 1
4Je, wewe una macho ya kimwili? 2 Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo? 1
5Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu, 2 au miaka yako ni kama ile ya mtu, 1
6ili kwamba utafute makosa yangu 2 na kuichunguza dhambi yangu; 1
7ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, 2 na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako? 1
8“Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya. 2 Je, sasa utageuka na kuniangamiza? 1
9Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. 2 Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena? 1
10Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa, 2 na kunigandisha kama jibini, 1
11ukanivika ngozi na nyama, 2 na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa? 1
12Umenipa uhai na kunitendea wema, 2 katika uangalizi wako umeilinda roho yangu. 1
13“Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako, 2 nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako: 1
14Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona, 2 wala usingeacha kosa langu lipite bila kuadhibiwa. 1
15Kama nina hatia, ole wangu! 2 Hata kama ningekuwa sina hatia, 2 siwezi kukiinua kichwa changu, 1 kwa kuwa nimejawa na aibu, 2 na kuzama katika mateso yangu. 1
16Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba, 2 na kuonyesha tena uwezo wa kutisha dhidi yangu. 1
17Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu 2 na kuzidisha hasira yako juu yangu; 2 nazo nguvu zako zinanijia wimbi moja baada ya jingine. 1
18“Kwa nini basi ulinitoa tumboni? 2 Ninatamani ningekufa kabla jicho lolote halijaniona. 1
19Laiti nisingekuwako kamwe, 2 au ningekuwa nimechukuliwa moja kwa moja 2 kutoka tumboni kwenda kaburini! 1
20Je, siku zangu chache si zimekaribia kuisha? 2 Niachie ili niweze kupata muda mfupi wa kufurahi 1
21kabla sijaenda mahali ambapo hakuna kurudi tena, 2 katika nchi ya giza na uvuli wa mauti, 1
22nchi ya giza kuu sana, 2 yenye uvuli wa giza na machafuko, 2 mahali ambapo hata nuru ni giza.”