Job · Biblia (Kiswahili)

Job 37

1“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, 2 nao unaruka kutoka mahali pake. 1

2Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, 2 sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake. 1

3Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote 2 na kuupeleka hata miisho ya dunia. 1

4Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; 2 Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. 1 Wakati sauti yake ingurumapo tena, 2 huuachilia umeme wake wa radi. 1

5Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; 2 yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu. 1

6Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ 2 nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’ 1

7Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, 2 yeye humzuilia kila mtu shughuli zake. 1

8Wanyama hujificha; 2 hubakia kwenye mapango yao. 1

9Dhoruba hutoka katika chumba chake, 2 baridi hutoka katika upepo uendao kasi. 1

10Pumzi ya Mungu hutoa barafu, 2 eneo kubwa la maji huganda. 1

11Huyasheheneza mawingu kwa maji, 2 naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo. 1

12Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, 2 juu ya uso wa dunia yote, 2 kufanya lolote ayaamuruyo. 1

13Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, 2 au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake. 1

14“Ayubu, sikiliza hili; 2 nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu. 1

15Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, 2 na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga? 1

16Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, 2 hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa? 1

17Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako 2 wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini, 1

18je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, 2 zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa? 1

19“Tuambieni yatupasayo kumwambia; 2 hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu. 1

20Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? 2 Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa? 1

21Basi hakuna awezaye kulitazama jua, 2 jinsi linavyongʼaa angani, 2 upepo ukishafagia mawingu. 1

22Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; 2 Mungu huja katika utukufu wa kutisha. 1

23Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; 2 katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea. 1

24Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, 2 kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

← Job 36Read In The App, Free →Job 38 →

Study Job 37

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142