Job 14
1“Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke 2 siku zake ni chache nazo zimejaa taabu. 1
2Huchanua kama ua kisha hunyauka; 2 huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu. 1
3Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? 2 Je, utamleta mbele yako katika hukumu? 1
4Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? 2 Hakuna awezaye! 1
5Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; 2 umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake 2 na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka. 1
6Hivyo angalia mbali umwache, 2 hadi awe amekamilisha muda wake 2 kama mtu aliyeajiriwa. 1
7“Kwa maana lipo tumaini kwa mti; 2 kama ukikatwa utachipuka tena, 2 nayo machipukizi yake mapya hayatakoma. 1
8Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini 2 na kisiki chake kufa udongoni, 1
9lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua 2 na kutoa machipukizi kama mche. 1
10Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; 2 hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena! 1
11Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, 2 au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu, 1
12ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; 2 hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, 1 wanadamu hawataamka au kuamshwa 2 kutoka kwenye usingizi wao. 1
13“Laiti kama ungenificha kaburini, + 14:13 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. 2 na kunisitiri hadi hasira yako ipite! 1 Laiti ungeniwekea wakati, 2 na kisha ukanikumbuka! 1
14Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? 2 Siku zote za kazi zangu ngumu 2 nitangojea kufanywa upya kwangu. 1
15Utaniita nami nitakuitika; 2 utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba. 1
16Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, 2 lakini hutazifuatia dhambi zangu. 1
17Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, 2 nawe utazifunika dhambi zangu. 1
18“Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika 2 na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake, 1
19kama maji yamalizavyo mawe, 2 na mafuriko yachukuavyo udongo, 2 ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu. 1
20Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; 2 waibadilisha sura yake na kumwondoa. 1
21Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; 2 kama wakidharauliwa, yeye haoni. 1
22Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, 2 naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”