Job 18
1Bildadi Mshuhi akajibu: 1
2“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? 2 Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea. 1
3Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, 2 na kuonekana wajinga machoni pako? 1
4Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande 2 katika hasira yako, 1 je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? 2 Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake? 1
5“Taa ya mwovu imezimwa, 2 nao mwali wa moto wake umezimika. 1
6Mwanga hemani mwake umekuwa giza; 2 taa iliyo karibu naye imezimika. 1
7Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; 2 shauri lake baya litamwangusha. 1
8Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, 2 naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu. 1
9Tanzi litamkamata kwenye kisigino; 2 mtego utamshikilia kwa nguvu. 1
10Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; 2 mtego uko kwenye njia yake. 1
11Vitisho vimemtia hofu kila upande, 2 na adui zake humwandama kila hatua. 1
12Janga linamwonea shauku; 2 maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo. 1
13Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; 2 mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake. 1
14Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, 2 na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho. 1
15Moto utakaa katika hema lake; 2 moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake. 1
16Mizizi yake chini itakauka 2 na matawi yake juu yatanyauka. 1
17Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, 2 wala hatakuwa na jina katika nchi. 1
18Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, 2 naye amefukuzwa mbali atoke duniani. 1
19Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, 2 wala aliyenusurika mahali alipoishi. 1
20Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; 2 watu wa mashariki watapatwa na hofu. 1
21Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; 2 ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”