Job · Biblia (Kiswahili)

Job 36

1Elihu akaendelea kusema: 1

2“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha 2 kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu. 1

3Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, 2 nami nitamhesabia haki Muumba wangu. 1

4Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; 2 mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe. 1

5“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; 2 ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake. 1

6Hawaachi waovu waendelee kuishi, 2 bali huwapa walioteswa haki yao. 1

7Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; 2 huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme 2 na kuwatukuza milele. 1

8Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, 2 wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso, 1

9huwaonyesha yale waliyoyatenda, 2 kwamba wametenda dhambi kwa majivuno. 1

10Huwafanya wao kusikia maonyo, 2 na huwaagiza kutubu uovu wao. 1

11Kama wakitii na kumtumikia, 2 wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, 2 na miaka yao katika utoshelevu. 1

12Lakini wasiposikiliza, 2 wataangamia kwa upanga, 2 nao watakufa pasipo maarifa. 1

13“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; 2 hata anapowafunga, hawamwombi msaada. 1

14Wanakufa wangali vijana, 2 miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu. 1

15Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, 2 na kuzungumza nao katika dhiki zao. 1

16“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, 2 ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, 2 hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri. 1

17Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; 2 hukumu na haki vimekukamata. 1

18Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; 2 usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa. 1

19Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi 2 vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki? 1

20Usiutamani usiku uje, 2 ili uwaburute watu mbali na nyumba zao. 1

21Jihadhari usigeukie uovu, 2 ambao unaupenda zaidi kuliko mateso. 1

22“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. 2 Ni nani aliye mwalimu kama yeye? 1

23Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, 2 au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’? 1

24Kumbuka kuzitukuza kazi zake, 2 ambazo watu wamezisifu katika wimbo. 1

25Wanadamu wote wameiona; 2 watu wanaikazia macho kwa mbali. 1

26Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, 2 kupita ufahamu wetu! 2 Hesabu ya miaka yake haitafutiki. 1

27“Yeye huvuta juu matone ya maji, 2 ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito; 1

28mawingu huangusha chini maji yake, 2 nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu. 1

29Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, 2 jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake. 1

30Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, 2 naye huvifunika vilindi vya bahari. 1

31Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, 2 na kuwapa chakula kwa wingi. 1

32Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, 2 na kuuagiza kulenga shabaha yake. 1

33Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; 2 hata mifugo hujulisha kukaribia kwake. + 36:33 Au: hutangaza kuja kwake.

← Job 35Read In The App, Free →Job 37 →

Study Job 36

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142