Job · Biblia (Kiswahili)

Job 9

1Kisha Ayubu akajibu: 1

2“Naam, najua hili ni kweli. 2 Lakini mwanadamu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu? 1

3Ingawa mtu angetaka kushindana naye, 2 asingaliweza kumjibu Mungu hata mara moja miongoni mwa elfu moja. 1

4Hekima yake ni kubwa sana na ana uwezo mwingi mno. 2 Ni nani aliyempinga naye akawa salama? 1

5Aiondoa milima bila yenyewe kujua 2 na kuipindua kwa hasira yake. 1

6Aitikisa dunia kutoka mahali pake 2 na kuzifanya nguzo zake zitetemeke. 1

7Husema na jua, nalo likaacha kuangaza; 2 naye huizima mianga ya nyota. 1

8Yeye peke yake huzitandaza mbingu 2 na kuyakanyaga mawimbi ya bahari. 1

9Yeye ndiye Muumba wa nyota za Dubu, + 9:9 Nyota za Dubu hapa ina maana ya kundi la nyota za kaskazini, ambazo zinaitwa kwa jina la Dubu Mkuu. na Orioni, + 9:9 Orioni ni kundi la nyota kubwa. 2 Kilimia, + 9:9 Kilimia ni jina lililopewa nyota saba (Taurus). na makundi ya nyota za kusini. 1

10Hutenda maajabu yasiyopimika, 2 miujiza isiyoweza kuhesabiwa. 1

11Anapopita karibu nami, siwezi kumwona; 2 apitapo mbele yangu, simtambui. 1

12Anapochukua kwa ghafula, ni nani awezaye kumzuia? 2 Ni nani awezaye kumwambia, ‘Unafanya nini?’ 1

13Mungu hataizuia hasira yake; 2 hata jeshi kubwa la Rahabu + 9:13 Rahabu hapa ina maana ya Misri kwa fumbo. lenye nguvu 2 linajikunyata miguuni pake. 1

14“Ni vipi basi mimi nitaweza kubishana naye? 2 Nawezaje kupata maneno ya kuhojiana naye? 1

15Ingawa sikuwa na hatia, sikuweza kumjibu; 2 ningeweza tu kumsihi Mhukumu wangu anihurumie. 1

16Hata kama ningemwita kwenye shauri, naye akakubali, 2 siamini kama angenisikiliza. 1

17Yeye angeniangamiza kwa dhoruba 2 na kuongeza majeraha yangu pasipo na sababu. 1

18Asingeniacha nipumue 2 bali angenifunika kabisa na huzuni kuu. 1

19Kama ni suala la nguvu, yeye ni mwenye nguvu! 2 Kama ni suala la haki, ni nani awezaye kumwita mahakamani? 1

20Hata kama sikuwa na hatia, kinywa changu kingenihukumu; 2 kama sikuwa na kosa, kingenitangaza kuwa mwenye hatia. 1

21“Ingawa mimi sina kosa, 2 haileti tofauti katika nafsi yangu; 2 nauchukia uhai wangu. 1

22Hayo yote ni sawa; ndiyo sababu nasema, 2 ‘Yeye huwaangamiza wasio na makosa pamoja na waovu.’ 1

23Wakati pigo liletapo kifo cha ghafula, 2 yeye hudhihaki kule kukata tamaa kwa yule asiye na kosa. 1

24Wakati nchi inapoangukia mikononi mwa waovu, 2 yeye huwafunga macho mahakimu wake. 2 Kama si yeye, basi ni nani? 1

25“Siku zangu zapita mbio kuliko mkimbiaji; 2 zinapita upesi bila kuona furaha hata kidogo. 1

26Zinapita upesi kama mashua ya mafunjo, 2 mfano wa tai ayashukiaye mawindo kwa ghafula. 1

27Kama nikisema, ‘Nitayasahau malalamiko yangu, 2 nitabadili sura ya uso wangu na kutabasamu,’ 1

28bado ninahofia mateso yangu yote, 2 kwa kuwa ninajua hutanihesabu kuwa sina hatia. 1

29Kwa kuwa nimeonekana mwenye hatia, 2 kwa nini basi nitaabishwe bure? 1

30Hata kama ningejiosha kwa sabuni 2 na kutakasa mikono yangu kwa magadi, 1

31wewe ungenitupa kwenye shimo la utelezi 2 kiasi kwamba hata nguo zangu zingenichukia sana. 1

32“Yeye si mwanadamu kama mimi ili niweze kumjibu, 2 ili kwamba tuweze kushindana naye mahakamani. 1

33Laiti angelikuwepo mtu wa kutupatanisha kati yetu, 2 aweke mkono wake juu yetu sote wawili, 1

34mtu angeliiondoa fimbo ya Mungu juu yangu, 2 ili utisho wake usiendelee kunitia hofu. 1

35Ndipo ningenena naye, bila kumwogopa, 2 lakini kama ilivyo kwangu sasa, sitaweza.

← Job 8Read In The App, Free →Job 10 →

Study Job 9

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142