Job · Biblia (Kiswahili)

Job 35

1Ndipo Elihu akasema: 1

2“Je, unadhani hili ni haki? 2 Wewe unasema, ‘Nina haki mbele za Mungu.’ 1

3Bado unamuuliza, ‘Ni faida gani nimepata, 2 na imenifaidi nini kwa kutokutenda dhambi?’ 1

4“Ningependa nikujibu wewe 2 pamoja na marafiki zako walio pamoja nawe. 1

5Tazama juu mbinguni ukaone; 2 yaangalie mawingu yaliyo juu sana juu yako. 1

6Je, ukitenda dhambi, inamdhuruje Mungu? 2 Kama dhambi zako zikiwa nyingi, 2 hilo linamfanyia nini Mungu? 1

7Kama wewe ni mwadilifu, unampa nini, 2 au yeye anapokea nini mkononi kwako? 1

8Uovu wako unamdhuru tu mtu mwingine kama wewe, 2 nayo haki yako inawafaa wanadamu tu. 1

9“Wanadamu hulia kwa kulemewa na mateso; 2 huomba msaada kutoka mkono wenye nguvu. 1

10Lakini hakuna asemaye, ‘Yuko wapi Mungu Muumba wangu, 2 yeye anifanyaye niimbe usiku, 1

11yeye atufundishaye sisi zaidi kuliko wanyama wa dunia, 2 na kutufanya wenye hekima kuliko ndege wa angani?’ 1

12Yeye hajibu wakati watu waliapo 2 kwa sababu ya kiburi cha watu waovu. 1

13Naam, Mungu hasikilizi maombi yao ya ubatili; 2 Mwenyezi hayazingatii. 1

14Si zaidi sana kwamba hatakusikiliza 2 wewe usemapo humwoni, 1 tena ya kwamba shauri lako liko mbele zake 2 na wewe lazima umngojee, 1

15pia zaidi, kwamba hasira yake kamwe haiadhibu 2 wala haangalii uovu hata kidogo? 1

16Hivyo Ayubu hufumbua kinywa chake kwa maneno yasiyo na maana; 2 anaongea maneno mengi bila maarifa.”

← Job 34Read In The App, Free →Job 36 →

Study Job 35

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142