Job 16
1Kisha Ayubu akajibu: 1
2“Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, 2 nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha! 1
3Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? 2 Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno? 1
4Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, 2 kama mngekuwa katika hali yangu; 1 ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, 2 na kuwatikisia ninyi kichwa changu. 1
5Lakini kinywa changu kingewatia moyo; 2 faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu. 1
6“Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; 2 nami kama nikijizuia, wala hayaondoki. 1
7Ee Mungu, hakika umenichakaza; 2 umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote. 1
8Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; 2 nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu. 1
9Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, 2 na kunisagia meno yake; 2 adui yangu hunikazia macho yake makali. 1
10Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; 2 hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, 2 na kuungana pamoja dhidi yangu. 1
11Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, 2 na kunitupa katika makucha ya waovu. 1
12Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; 2 amenikamata shingo na kuniponda. 2 Amenifanya mimi kuwa shabaha yake; 1
13wapiga upinde wake wananizunguka. 2 Bila huruma, huchoma figo zangu, 2 na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi. 1
14Huniponda tena na tena; 2 hunishambulia kama shujaa wa vita. 1
15“Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu 2 nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi. 1
16Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, 2 macho yangu yamepigwa na giza kuu. 1
17Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, 2 na maombi yangu ni safi. 1
18“Ee nchi, usiifunike damu yangu, 2 nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe. 1
19Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; 2 wakili wangu yuko juu. 1
20Mwombezi wangu ni rafiki yangu 2 macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu; 1
21kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu 2 kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake. 1
22“Ni miaka michache tu itapita 2 kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.