Job 19
1Ndipo Ayubu akajibu: 1
2“Je, mtaendelea kunitesa mpaka lini, 2 na kuniponda kwa maneno yenu? 1
3Mara kumi hizi mmenishutumu; 2 bila aibu mnanishambulia. 1
4Kama ni kweli nimepotoka, 2 kosa langu ninabaki kuhusika nalo mwenyewe. 1
5Kama kweli mngejitukuza wenyewe juu yangu, 2 na kutumia unyonge wangu dhidi yangu, 1
6basi jueni kuwa Mungu amenitendea yaliyo mabaya, 2 naye amekokota wavu wake kunizunguka. 1
7“Ingawa ninalia, ‘Nimetendewa mabaya!’ sipati jibu; 2 ingawa ninaomba msaada, hakuna haki. 1
8Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita; 2 ameyafunika mapito yangu na giza. 1
9Amenivua heshima yangu, 2 na kuniondolea taji kichwani pangu. 1
10Amenibomoa kila upande hadi nimeisha; 2 amelingʼoa tegemeo langu kama mti. 1
11Hasira yake imewaka juu yangu; 2 amenihesabu kuwa miongoni mwa adui zake. 1
12Majeshi yake yananisogelea kwa nguvu; 2 yamenizingira, 2 yamepiga kambi kulizunguka hema langu. 1
13“Amewatenga ndugu zangu mbali nami; 2 wale tunaojuana nao wamefarakana nami kabisa. 1
14Watu wa jamaa yangu wamekwenda mbali; 2 rafiki zangu wamenisahau. 1
15Wageni wangu na watumishi wangu wa kike wananiona kama mgeni; 2 wananitazama kama mgeni. 1
16Namwita mtumishi wangu, wala haitiki, 2 ingawa namwomba kwa kinywa changu mwenyewe. 1
17Pumzi ya kinywa changu ni kinyaa kwa mke wangu; 2 nimekuwa chukizo mno kwa ndugu zangu mwenyewe. 1
18Hata watoto wadogo hunidhihaki; 2 ninapojitokeza, hunifanyia mzaha. 1
19Rafiki zangu wa moyoni wote wananichukia kabisa; 2 wale niwapendao wamekuwa kinyume nami. 1
20Mimi nimebaki mifupa na ngozi tu; 2 nimeponea nikiwa karibu kufa. 1
21“Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma, 2 kwa kuwa mkono wa Mungu umenipiga. 1
22Kwa nini mnanifuatia kama Mungu afanyavyo? 2 Hamtosheki kamwe na mwili wangu? 1
23“Laiti maneno yangu yangewekwa kwenye kumbukumbu, 2 laiti kwamba yangeandikwa kwenye kitabu, 1
24kwamba yangechorwa kwenye risasi kwa kifaa cha chuma, 2 au kuyachonga juu ya mwamba milele! 1
25Ninajua kwamba Mkombozi + 19:25 Au: Mtetezi. wangu yu hai, 2 naye kwamba mwishoni atasimama juu ya nchi. 1
26Nami baada ya ngozi yangu kuharibiwa, 2 bado nikiwa na mwili huu nitamwona Mungu; 1
27mimi nitamwona kwa macho yangu mwenyewe: 2 mimi, wala si mwingine. 2 Tazama jinsi moyo wangu unavyomtamani sana! 1
28“Kama mkisema, ‘Tazama tutakavyomwinda, 2 maadamu mzizi wa tatizo uko ndani yake,’ 1
29ninyi wenyewe uogopeni upanga, 2 kwa kuwa ghadhabu italeta adhabu kwa upanga, 2 nanyi ndipo mtakapojua kwamba kuna hukumu.”