Job · Biblia (Kiswahili)

Job 28

1“Kuna machimbo ya fedha, 2 na mahali dhahabu isafishwapo. 1

2Chuma hupatikana ardhini, 2 nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini. 1

3Mwanadamu hukomesha giza; 2 huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, 1 kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini 2 katika giza jeusi sana. 1

4Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, 2 mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; 2 mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba. 1

5Ardhi, ambako chakula hutoka, 2 chini hugeuzwa kwa moto; 1

6yakuti samawi hutoka katika miamba yake, 2 nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu. 1

7Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, 2 wala hakuna jicho la mwewe lililoiona. 1

8Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, 2 wala simba azungukaye huko. 1

9Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, 2 na kuiacha wazi mizizi ya milima. 1

10Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; 2 macho yake huona hazina zake zote. 1

11Hutafuta vyanzo vya mito 2 na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru. 1

12“Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? 2 Ufahamu unakaa wapi? 1

13Mwanadamu hatambui thamani yake; 2 haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai. 1

14Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; 2 bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’ 1

15Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, 2 wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha. 1

16Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, 2 kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa. 1

17Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, 2 wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu. 1

18Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; 2 thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu. 1

19Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, 2 wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi. 1

20“Ni wapi basi hekima itokako? 2 Ufahamu hukaa wapi? 1

21Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, 2 imesitiriwa hata kwa ndege wa angani. 1

22Uharibifu na Mauti husema, 2 ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’ 1

23Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima 2 na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa, 1

24kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia 2 na huona kila kitu chini ya mbingu. 1

25Alipofanyiza nguvu za upepo 2 na kuyapima maji, 1

26alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua 2 na njia kwa ajili ya umeme wa radi, 1

27ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, 2 akaithibitisha na kuihakikisha. 1

28Naye Mungu akamwambia mwanadamu, 2 ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, 2 nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’ ”

← Job 27Read In The App, Free →Job 29 →

Study Job 28

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142