Job 4
1Ndipo Elifazi Mtemani akajibu: 1
2“Kama mtu akithubutu kuzungumza nawe, 2 kutakukasirisha? 1 Lakini ni nani awezaye 2 kujizuia asiseme? 1
3Fikiri jinsi ambavyo umewafundisha watu wengi, 2 jinsi ambavyo umeitia nguvu 2 mikono iliyokuwa dhaifu. 1
4Maneno yako yamewategemeza wale waliojikwaa; 2 umeyatia nguvu magoti yaliyokuwa dhaifu. 1
5Lakini sasa hii taabu imekujia wewe, 2 nawe unashuka moyo; 1 imekupiga wewe, 2 nawe unafadhaika. 1
6Je, kumcha Mungu kwako hakupaswi kuwa 2 ndiyo matumaini yako 1 na njia zako kutokuwa na lawama 2 ndilo taraja lako? 1
7“Fikiri sasa: Ni mtu yupi asiye na hatia ambaye aliwahi kuangamia? 2 Ni wapi wanyofu waliwahi kuangamizwa? 1
8Kwa jinsi ambavyo mimi nimechunguza, 2 wale walimao ubaya 1 na wale hupanda uovu, 2 huvuna hayo hayo hayo. 1
9Kwa pumzi ya Mungu huangamizwa; 2 kwa mshindo wa hasira zake huangamia. 1
10Simba anaweza kunguruma na kukoroma, 2 lakini bado meno ya simba mkubwa huvunjika. 1
11Simba anaweza kuangamia kwa kukosa mawindo, 2 nao wana wa simba jike hutawanyika. 1
12“Neno lililetwa kwangu kwa siri, 2 masikio yangu yakasikia mnongʼono wake. 1
13Katikati ya ndoto za kutia wasiwasi wakati wa usiku, 2 hapo usingizi mzito uwapatapo wanadamu, 1
14hofu na kutetemeka kulinishika 2 na kufanya mifupa yangu yote itetemeke. 1
15Kuna roho aliyepita mbele ya uso wangu, 2 nazo nywele za mwili wangu zikasimama. 1
16Yule roho akasimama, 2 lakini sikuweza kutambua kilikuwa kitu gani. 1 Umbo fulani lilisimama mbele ya macho yangu, 2 kukawa na ukimya kisha nikasikia sauti: 1
17‘Je, binadamu aweza kuwa mwadilifu kuliko Mungu? 2 Je, mtu aweza kuwa safi kuliko Muumba wake? 1
18Kama Mungu hawaamini watumishi wake, 2 kama yeye huwalaumu malaika zake kwa kukosea, 1
19ni mara ngapi zaidi wale waishio katika nyumba 2 za udongo wa mfinyanzi, 1 ambazo misingi yake ipo mavumbini, 2 ambao wamepondwa kama nondo! 1
20Kati ya mawio na machweo 2 huvunjwa vipande vipande; 1 bila yeyote kutambua, 2 huangamia milele. 1
21Je, kamba za hema yao hazikungʼolewa, 2 hivyo hufa bila hekima?’