Job 21
1Ndipo Ayubu akajibu: 1
2“Yasikilizeni maneno yangu kwa makini; 2 hii na iwe faraja mnayonipa mimi. 1
3Nivumilieni ninapozungumza, 2 nami nikishazungumza, endeleeni kunidhihaki. 1
4“Je, kwani malalamiko yangu yanaelekezwa kwa mwanadamu? 2 Kwa nini nisikose subira? 1
5Niangalieni mkastaajabu; 2 mkaweke mkono juu ya vinywa vyenu. 1
6Ninapowaza juu ya hili, ninaogopa, 2 nao mwili wangu unatetemeka. 1
7Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, 2 wakifikia umri wa uzee na kuendelea kuwa na nguvu? 1
8Huwaona watoto wao wakithibitika 2 wakiwa wamewazunguka, 2 wazao wao mbele za macho yao. 1
9Nyumba zao zi salama wala hakuna hofu; 2 fimbo ya Mungu haiko juu yao. 1
10Madume yao ya ngʼombe huvyaza bila kushindwa kamwe; 2 ngʼombe wao huzaa wala hawaharibu mimba. 1
11Huwatoa watoto wao nje kama kundi; 2 wadogo wao huchezacheza. 1
12Huimba nyimbo kwa matari na kwa kinubi, 2 nao huifurahia sauti ya filimbi. 1
13Huitumia miaka yao katika mafanikio 2 nao hushuka kaburini kwa amani. 1
14Lakini humwambia Mungu, ‘Tuache sisi!’ 2 Hatuna haja ya kufahamu njia zako. 1
15Mwenyezi ni nani hata tumtumikie? 2 Tutapata faida gani kumwomba? 1
16Lakini kufanikiwa kwao hakupo mikononi mwao wenyewe, 2 hivyo najitenga mbali na shauri la waovu. 1
17“Lakini ni mara ngapi taa ya waovu huzimwa? 2 Ni mara ngapi maafa huwajia, 1 yale yawapatayo ambayo Mungu 2 huwapangia katika hasira yake? 1
18Ni mara ngapi huwa kama majani makavu mbele ya upepo, 2 kama makapi yachukuliwayo na dhoruba? 1
19Imesemekana, ‘Mungu huiweka akiba adhabu ya mtu 2 kwa ajili ya wanawe.’ 1 Mungu na amlipe mtu mwenyewe, 2 ili apate kulijua! 1
20Macho yake mwenyewe na yaone maangamizi yake; 2 yeye na ainywe ghadhabu ya Mwenyezi. 1
21Kwani anajali nini kuhusu jamaa anayoiacha nyuma, 2 miezi yake aliyopangiwa ifikapo mwisho? 1
22“Je, yuko mtu yeyote awezaye kumfundisha Mungu maarifa, 2 iwapo yeye ndiye ahukumuye hata walio juu ya wote? 1
23Mtu mmoja hufa akiwa na nguvu zake kamili, 2 akiwa salama na mwenye raha kamili, 1
24mwili wake ukiwa umenawiri, 2 nayo mifupa yake ikiwa imejaa mafuta ndani yake. 1
25Mtu mwingine hufa katika uchungu wa nafsi, 2 akiwa hajafurahia kamwe jambo lolote zuri. 1
26Hao wote hulala mavumbini, 2 nao mabuu huwafunika wote. 1
27“Ninayajua kikamilifu yale mnayoyafikiri, 2 mipango ambayo kwayo mngenitendea mabaya. 1
28Mwasema, ‘Iko wapi sasa nyumba ya huyo mtu mkuu, 2 mahema ambayo watu waovu walikaa?’ 1
29Je, hamkuwahi kuwauliza hao wanaosafiri? 2 Je, hamkutafakari taarifa zao: 1
30kwamba mtu mwovu huepushwa kutoka siku ya maafa, 2 kwamba huokolewa kutoka siku ya ghadhabu? 1
31Ni nani hulaumu matendo yake mbele ya uso wake? 2 Ni nani ampatilizaye kwa yale aliyoyatenda? 1
32Hupelekwa kaburini, 2 nao ulinzi ukawekwa kwenye kaburi lake. 1
33Udongo ulio bondeni ni mtamu kwake; 2 watu wote watamfuata, 2 nao umati wa watu usiohesabika umemtangulia. 1
34“Hivyo ninyi mnawezaje kunifariji kwa upuzi wenu? 2 Hakuna kilichosalia cha majibu yenu isipokuwa uongo!”