Job · Biblia (Kiswahili)

Job 27

1Ndipo Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema: 1

2“Hakika kama Mungu aishivyo, aliyeninyima haki yangu, 2 Mwenyezi ambaye amenifanya 2 nionje uchungu wa nafsi, 1

3kwa muda wote nitakaokuwa na uhai ndani yangu, 2 nayo pumzi ya Mungu ikiwa puani mwangu, 1

4midomo yangu haitanena uovu, 2 wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu. 1

5Sitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi; 2 hadi nife, sitakana uadilifu wangu. 1

6Nitadumisha haki yangu wala sitaiacha; 2 dhamiri yangu haitanisuta muda wote ninaoishi. 1

7“Watesi wangu wawe kama waovu, 2 nao adui zangu wawe kama wasio haki! 1

8Kwa maana mtu asiyemcha Mungu 2 analo tegemeo gani anapokatiliwa mbali, 2 Mungu anapouondoa uhai wake? 1

9Je, Mungu husikiliza kilio chake, 2 shida zimjiapo? 1

10Je, anaweza kumfurahia Mwenyezi? 2 Je, atamwita Mungu nyakati zote? 1

11“Nitawafundisha juu ya uweza wa Mungu; 2 njia za Mwenyezi sitazificha. 1

12Ninyi nyote mmeona hili wenyewe. 2 Ni ya nini basi mazungumzo haya yasiyo na maana? 1

13“Hili ndilo fungu ambalo Mungu humpa mtu mwovu, 2 urithi ule mtu mdhalimu anapokea kutoka kwa Mwenyezi: 1

14Hata kama watoto wake watakuwa wengi kiasi gani, 2 fungu lao ni kuuawa kwa upanga; 1 wazao wake hawatakuwa kamwe 2 na chakula cha kuwatosha. 1

15Tauni itawazika wale watakaonusurika miongoni mwao, 2 nao wajane wao hawatawaombolezea. 1

16Ajapokusanya fedha nyingi kama mavumbi, 2 na mavazi kama malundo ya udongo wa mfinyanzi, 1

17yale yote mtu mwovu aliyojiwekea akiba, mwenye haki atayavaa, 2 naye asiye na hatia ataigawanya fedha yake. 1

18Nyumba aijengayo ni kama utando wa buibui, 2 kama kibanda alichotengeneza mlinzi. 1

19Yeye hulala akiwa tajiri, lakini ndiyo mara ya mwisho; 2 afunguapo macho yake, yote yametoweka. 1

20Vitisho humjia kama mafuriko; 2 dhoruba humkumba ghafula usiku. 1

21Upepo mkali wa mashariki humchukua, naye hutoweka; 2 humzoa kutoka mahali pake. 1

22Humvurumisha bila huruma, 2 huku akikimbia kasi kukwepa nguvu zake. 1

23Upepo humpigia makofi kwa dharau, 2 na kumfukuza atoke mahali pake.

← Job 26Read In The App, Free →Job 28 →

Study Job 27

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142