Job · Biblia (Kiswahili)

Job 23

1Ndipo Ayubu akajibu: 1

2“Hata leo malalamiko yangu ni chungu; 2 mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua. 1

3Laiti ningefahamu mahali pa kumwona; 2 laiti ningeweza kwenda mahali akaapo! 1

4Ningeliweka shauri langu mbele zake, 2 na kukijaza kinywa changu na hoja. 1

5Ningejua kwamba angenijibu nini, 2 na kuelewa lile ambalo angelisema. 1

6Je, angenipinga kwa nguvu nyingi? 2 La, asingenigandamiza. 1

7Hapo mtu mwadilifu angeweka shauri lake mbele zake, 2 nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu. 1

8“Lakini nikienda mashariki, hayupo; 2 nikienda magharibi, simpati. 1

9Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni; 2 akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo. 1

10Lakini anaijua njia niiendeayo; 2 akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu. 1

11Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu; 2 nimeishika njia yake bila kukengeuka. 1

12Sijaziacha amri zilizotoka midomoni mwake; 2 nimeyathamini maneno ya kinywa chake kuliko chakula changu cha kila siku. 1

13“Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga? 2 Yeye hufanya lolote atakalo. 1

14Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu, 2 na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba. 1

15Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake; 2 nifikiriapo haya yote ninamwogopa. 1

16Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia; 2 yeye Mwenyezi amenitia hofu. 1

17Hata hivyo sijanyamazishwa na giza, 2 wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.

← Job 22Read In The App, Free →Job 24 →

Study Job 23

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142