Job 22
1Ndipo Elifazi Mtemani akajibu: 1
2“Je, mwanadamu aweza kuwa wa faida kwa Mungu? 2 Je, hata mtu mwenye hekima aweza kumfaidi? 1
3Je, Mwenyezi angefurahia nini 2 kama ungekuwa mwadilifu? 1 Au je, yeye angepata faida gani 2 kama njia zako zingekuwa kamilifu? 1
4“Je, ni kwa ajili ya utaua wako ndiyo maana anakukemea 2 na kuleta mashtaka dhidi yako? 1
5Je, uovu wako si mkuu? 2 Dhambi zako si hazina mwisho? 1
6Umedai dhamana kwa ndugu zako bila sababu; 2 umewavua watu nguo zao, ukawaacha uchi. 1
7Hukumpa maji aliyechoka, 2 nawe ulimnyima chakula mwenye njaa, 1
8ingawa ulikuwa mtu mwenye uwezo ukimiliki nchi: 2 mtu uliyeheshimiwa, ukiishi ndani yake. 1
9Umewafukuza wajane mikono mitupu 2 na kuzivunja nguvu za yatima. 1
10Ndiyo sababu mitego imekuzunguka pande zote, 2 hatari ya ghafula inakutia hofu, 1
11ndiyo sababu ni giza sana huwezi kuona, 2 tena ndiyo sababu mafuriko ya maji yamekufunika. 1
12“Je, Mungu hayuko katika mbingu za juu? 2 Juu kuliko nyota zilizo juu sana! 1
13Hivyo wewe wasema, ‘Mungu anajua nini?’ 2 Je, yeye huhukumu katika giza kama hilo? 1
14Mawingu mazito ni pazia lake, hivyo hatuoni sisi 2 atembeapo juu ya anga la dunia. 1
15Je, utaifuata njia ya zamani, 2 ambayo watu waovu waliikanyaga? 1
16Waliondolewa kabla ya wakati wao, 2 misingi yao ikachukuliwa na mafuriko. 1
17Walimwambia Mungu, ‘Tuache sisi! 2 Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?’ 1
18Lakini ndiye alizijaza nyumba zao na vitu vizuri, 2 hivyo ninajitenga mbali na mashauri ya waovu. 1
19“Wenye haki wanaona maangamizi yao na kufurahi, 2 nao wasio na hatia huwadhihaki, wakisema, 1
20‘Hakika adui zetu wameangamizwa, 2 nao moto umeteketeza mali zao.’ 1
21“Mjue sana Mungu ili uwe na amani, 2 ndipo mema yatakapokujia. 1
22Uyapokee mafundisho toka kinywani mwake, 2 na maneno yake uyaweke moyoni mwako. 1
23Kama ukimrudia Mwenyezi, utarudishwa upya: 2 Kama ukiuondoa uovu uwe mbali na hema lako, 1
24kama dhahabu yako ukiihesabu kama mavumbi, 2 dhahabu yako ya Ofiri kama miamba ya mabondeni, 1
25ndipo Mwenyezi atakuwa dhahabu yako, 2 naye atakuwa fedha yako iliyo bora. 1
26Hakika ndipo utakapojifurahisha kwa Mwenyezi, 2 nawe utamwinulia Mungu uso wako. 1
27Utamwomba yeye, naye atakusikia, 2 nawe utazitimiza nadhiri zako. 1
28Utakusudia jambo nalo litatendeka, 2 nao mwanga utaangazia njia zako. 1
29Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’ 2 ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo. 1
30Atamwokoa hata yule ambaye ana hatia, 2 ataokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.”