Job · Biblia (Kiswahili)

Job 17

1Moyo wangu umevunjika, 2 siku zangu zimefupishwa, 2 kaburi linaningojea. 1

2Hakika wenye mizaha wamenizunguka; 2 macho yangu yamebaki kutazama uadui wao. 1 Ayubu Anaomba Msaada 1

3“Ee Mungu, nipe dhamana unayodai. 2 Ni nani mwingine atakayeweka dhamana kwa ajili yangu? 1

4Umezifunga akili zao zisipate ufahamu, 2 kwa hiyo hutawaacha wapate ushindi. 1

5Kama mtu akiwashutumu rafiki zake ili apate ujira, 2 macho ya watoto wake yatashindwa kuona. 1

6“Mungu amenifanya kitu cha dhihaka kwa kila mtu, 2 mtu ambaye watu humtemea mate usoni. 1

7Macho yangu yamefifia kwa ajili ya majonzi; 2 umbile langu lote ni kama kivuli. 1

8Watu wanyofu wanatishwa na hili; 2 watu wasio na hatia wanasimama dhidi ya wasiomcha Mungu. 1

9Hata hivyo, waadilifu watazishika njia zao, 2 nao wale wenye mikono safi wataendelea kupata nguvu. 1

10“Lakini ninyi njooni, ninyi nyote, jaribuni tena! 2 Sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu. 1

11Siku zangu zimepita, mipango yangu imevunjika, 2 vivyo hivyo shauku za moyo wangu. 1

12Watu hawa hufanya usiku kuwa mchana, 2 kwenye giza wao husema, ‘Mwanga u karibu.’ 1

13Kama nyumba pekee ninayoitarajia ni kaburi, + 17:13 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. 2 kama nikikitandika kitanda changu gizani, 1

14kama nikiuambia uharibifu, ‘Wewe u baba yangu,’ 2 na kuliambia buu, ‘Wewe u mama yangu’ au ‘Dada yangu,’ 1

15liko wapi basi tarajio langu? 2 Ni nani awezaye kuona tarajio lolote kwa ajili yangu? 1

16Je, litashuka chini hadi kwenye malango ya mauti? + 17:16 Malango ya mauti hapa ina maana ya Kuzimu. 2 Je, tutashuka pamoja mavumbini?”

← Job 16Read In The App, Free →Job 18 →

Study Job 17

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142