Job · Biblia (Kiswahili)

Job 41

1“Je, waweza kumvua Lewiathani + 41:1 Lewiathani ni mnyama mkubwa wa baharini mwenye magamba anayefanana na joka kubwa, mwenye umbo la kutisha, asiyeweza kuvuliwa. kwa ndoano ya samaki, 2 au kufunga ulimi wake kwa kamba? 1

2Waweza kupitisha kamba puani mwake, 2 au kutoboa taya lake kwa kulabu? 1

3Je, ataendelea kukuomba umhurumie? 2 Atasema nawe maneno ya upole? 1

4Je, atafanya agano nawe ili umtwae 2 awe mtumishi wako maisha yake yote? 1

5Je, utamfuga na kumfanya rafiki kama ndege, 2 au kumfunga kamba kwa ajili ya wasichana wako? 1

6Je, wafanyabiashara watabadilishana bidhaa kwa ajili yake? 2 Watamgawanya miongoni mwa wafanyao biashara? 1

7Je, waweza kuijaza ngozi yake kwa vyuma vyenye ncha kali, 2 au kichwa chake kwa mkuki wa kuvulia samaki? 1

8Kama ukiweka mkono wako juu yake, 2 utavikumbuka hivyo vita na kamwe hutarudia tena! 1

9Tumaini lolote la kumtiisha ni kujidanganya; 2 kule kumwona tu kunamwangusha mtu chini. 1

10Hakuna yeyote aliye mkali athubutuye kumchokoza. 2 Ni nani basi awezaye kusimama dhidi yangu? 1

11Ni nani mwenye madai dhidi yangu ili nipate kumlipa? 2 Kila kitu kilicho chini ya mbingu ni mali yangu. 1

12“Sitashindwa kunena juu ya maungo yake, 2 nguvu zake na umbo lake zuri. 1

13Ni nani awezaye kumvua gamba lake la nje? 2 Ni nani awezaye kumsogelea na lijamu? 1

14Nani athubutuye kuufungua mlango wa kinywa chake, 2 kilichozungukwa na meno yake ya kutisha pande zote? 1

15Mgongo wake una safu za ngao 2 zilizoshikamanishwa imara pamoja; 1

16kila moja iko karibu sana na mwenzake, 2 wala hakuna hewa iwezayo kupita kati yake. 1

17Zimeunganishwa imara kila moja na nyingine; 2 zimengʼangʼaniana pamoja wala haziwezi kutenganishwa. 1

18Akipiga chafya mwanga humetameta; 2 macho yake ni kama mionzi ya mapambazuko. 1

19Mienge iwakayo humiminika kutoka kinywani mwake; 2 cheche za moto huruka nje. 1

20Moshi hufuka kutoka puani mwake, 2 kama kutoka kwenye chungu kinachotokota kwa moto wa matete. 1

21Pumzi yake huwasha makaa ya mawe, 2 nayo miali ya moto huruka kutoka kinywani mwake. 1

22Nguvu hukaa katika shingo yake; 2 utisho hutangulia mbele yake. 1

23Mikunjo ya nyama yake imeshikamana imara pamoja; 2 iko imara na haiwezi kuondolewa. 1

24Kifua chake ni kigumu kama mwamba, 2 kigumu kama jiwe la chini la kusagia. 1

25Ainukapo, mashujaa wanaogopa; 2 hurudi nyuma mbele yake anapokwenda kwa kishindo. 1

26Upanga unaomfikia haumdhuru, 2 wala mkuki au mshale wala fumo. 1

27Chuma hukiona kama unyasi, 2 na shaba kama mti uliooza. 1

28Mishale haimfanyi yeye akimbie; 2 mawe ya kombeo kwake ni kama makapi. 1

29Rungu kwake huwa kama kipande cha jani kavu; 2 hucheka sauti za kugongana kwa mkuki. 1

30Sehemu zake za chini kwenye tumbo 2 zina menomeno na mapengo kama vigae vya chungu, 1 zikiacha mburuzo kwenye matope 2 kama chombo chenye meno cha kupuria. 1

31Huvisukasuka vilindi kama sufuria kubwa ichemkayo, 2 na kukoroga bahari kama chungu cha marhamu. 1

32Anapopita nyuma yake huacha mkondo unaometameta; 2 mtu angedhani vilindi vilikuwa na mvi. 1

33Hakuna chochote duniani kinacholingana naye: 2 yeye ni kiumbe kisicho na woga. 1

34Yeye huwatazama chini wale wote wenye kujivuna; 2 yeye ni mfalme juu ya wote wenye kiburi.”

← Job 40Read In The App, Free →Job 42 →

Study Job 41

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142