Job 13
1“Macho yangu yameona hili lote, 2 masikio yangu yamesikia na kulielewa. 1
2Hayo mnayoyajua mimi pia ninayajua; 2 mimi si mtu duni kuliko ninyi. 1
3Lakini ninayo shauku ya kuzungumza na Mwenyezi 2 na kuhojiana shauri langu na Mungu. 1
4Ninyi, hata hivyo, hunipakaza uongo; 2 ninyi ni matabibu wasiofaa kitu, ninyi nyote! 1
5Laiti wote mngenyamaza kimya! 2 Kwa kuwa kwenu hilo lingekuwa hekima. 1
6Sikieni sasa hoja yangu; 2 sikilizeni kusihi kwangu. 1
7Je, mtazungumza kwa uovu kwa niaba ya Mungu? 2 Je, mtazungumza kwa udanganyifu kwa niaba yake? 1
8Mtamwonyesha upendeleo? 2 Mtamtetea Mungu kwenye mashtaka yake? 1
9Je, ingekuwa vyema Mungu akiwahoji ninyi? 2 Je, mngeweza kumdanganya kama ambavyo mngeweza kuwadanganya wanadamu? 1
10Hakika angewakemea 2 kama mkiwapendelea watu kwa siri. 1
11Je, huo ukuu wake haungewatisha ninyi? 2 Je, hofu yake isingewaangukia ninyi? 1
12Maneno yenu ni mithali za majivu; 2 utetezi wenu ni ngome za udongo wa mfinyanzi. 1
13“Nyamazeni kimya nipate kusema; 2 kisha na yanipate yatakayonipata. 1
14Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari 2 na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu? 1
15Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; 2 hakika nitazitetea njia zangu mbele zake. 1
16Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, 2 kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu 2 atakayethubutu kuja mbele yake! 1
17Sikilizeni maneno yangu kwa makini; 2 nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho. 1
18Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, 2 ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki. 1
19Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? 2 Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife. 1
20“Ee Mungu, unijalie tu mimi haya mambo mawili, 2 nami sitajificha uso wako: 1
21Ondoa mkono wako uwe mbali nami, 2 nawe uache kuniogofya kwa hofu zako kuu. 1
22Niite kwenye shauri nami nitajibu, 2 au niache niseme, nawe upate kujibu. 1
23Ni makosa na dhambi ngapi nilizotenda? 2 Nionyeshe kosa langu na dhambi yangu. 1
24Kwa nini kuuficha uso wako 2 na kunihesabu mimi kuwa adui yako? 1
25Je, utaliadhibu jani lipeperushwalo na upepo? 2 Je, utayasaka makapi makavu? 1
26Kwa kuwa unaandika mambo machungu dhidi yangu 2 na kunifanya nizirithi dhambi za ujana wangu. 1
27Umeifunga miguu yangu kwenye pingu. 2 Unazichunga kwa makini njia zangu zote 2 kwa kutia alama kwenye nyayo za miguu yangu. 1
28“Hivyo mwanadamu huangamia kama kitu kilichooza, 2 kama vazi lililoliwa na nondo.