Job · Biblia (Kiswahili)

Job 38

1Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema: 1

2“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza 2 kwa maneno yasiyo na maarifa? 1

3Jikaze kama mwanaume; 2 nitakuuliza swali, 2 nawe unijibu. 1

4“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? 2 Niambie, kama unafahamu. 1

5Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? 2 Hakika wewe unajua! 2 Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake? 1

6Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, 2 au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni, 1

7wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, 2 na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha? 1

8“Ni nani aliyeifungia bahari milango 2 ilipopasuka kutoka tumbo, 1

9nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, 2 na kuyafungia katika giza nene, 1

10nilipoamuru mipaka yake, 2 na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake, 1

11niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; 2 hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’? 1

12“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, 2 au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake, 1

13yapate kushika miisho ya dunia, 2 na kuwakungʼuta waovu waliomo? 1

14Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; 2 sura yake hukaa kama ile ya vazi. 1

15Waovu huzuiliwa nuru yao, 2 nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa. 1

16“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? 2 Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi? 1

17Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? 2 Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti? 1

18Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? 2 Niambie kama unajua haya yote. 1

19“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? 2 Nako maskani mwa giza ni wapi? 1

20Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? 2 Unajua njia za kufika maskani mwake? 1

21Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! 2 Kwani umeishi miaka mingi! 1

22“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, 2 au kuona ghala za mvua ya mawe, 1

23ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, 2 na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano? 1

24Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, 2 au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia? 1

25Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi 2 na njia ya umeme wa radi, 1

26ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, 2 jangwa lisilo na yeyote ndani yake, 1

27ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, 2 na majani yaanze kumea ndani yake? 1

28Je, mvua ina baba? 2 Ni nani baba azaaye matone ya umande? 1

29Barafu inatoka tumbo la nani? 2 Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni, 1

30wakati maji yawapo magumu kama jiwe, 2 wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda? 1

31“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? 2 Waweza kulegeza kamba za Orioni? 1

32Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, 2 au kuongoza Dubu na watoto wake? 1

33Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? 2 Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani? 1

34“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, 2 na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji? 1

35Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? 2 Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’? 1

36Ni nani aliyeujalia moyo hekima 2 au kuzipa akili ufahamu? 1

37Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? 2 Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni 1

38wakati mavumbi yawapo magumu, 2 na mabonge ya udongo kushikamana pamoja? 1

39“Je, utamwindia simba jike mawindo, 2 na kuwashibisha simba wenye njaa 1

40wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, 2 au wakivizia kichakani? 1

41Ni nani ampaye kunguru chakula 2 wakati makinda yake yanamlilia Mungu, 2 yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

← Job 37Read In The App, Free →Job 39 →

Study Job 38

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142