Isaiah · Biblia (Kiswahili)

Isaiah 12

1Katika siku ile utasema: 1 “Nitakusifu wewe, Ee Bwana. 2 Ingawa ulinikasirikia, 1 hasira yako imegeukia mbali 2 nawe umenifariji. 1

2Hakika Mungu ni wokovu wangu; 2 nitamtumaini wala sitaogopa. 1 Bwana, Bwana, ni nguvu zangu na wimbo wangu; 2 amekuwa wokovu wangu.” 1

3Kwa furaha mtachota maji 2 kutoka visima vya wokovu.

4Katika siku hiyo mtasema: 1 “Mshukuruni Bwana, mliitie jina lake; 2 julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya, 2 tangazeni kuwa jina lake limetukuka. 1

5Mwimbieni Bwana, kwa kuwa ametenda mambo makuu, 2 hili na lijulikane duniani kote. 1

6Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni, 2 kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”

← Isaiah 11Read In The App, Free →Isaiah 13 →

Study Isaiah 12

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566