Isaiah · Biblia (Kiswahili)

Isaiah 26

1Katika siku ile, wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda: 1 Tuna mji ulio na nguvu, 2 Mungu huufanya wokovu kuwa kuta zake na maboma yake. 1

2Fungua malango ili taifa lenye haki lipate kuingia, 2 taifa lile lidumishalo imani. 1

3Utamlinda katika amani kamilifu 2 yeye ambaye moyo wake ni thabiti 2 kwa sababu anakutumaini wewe. 1

4Mtumaini Bwana milele, 2 kwa kuwa Bwana, Bwana, ni Mwamba wa milele. 1

5Huwashusha wale wajikwezao, 2 huushusha chini mji wenye kiburi, 1 huushusha hadi ardhini 2 na kuutupa chini mavumbini. 1

6Miguu huukanyaga chini, 2 miguu ya hao walioonewa, 2 hatua za hao maskini. 1

7Mapito ya wenye haki yamenyooka. 2 Ewe uliye Mwenye Haki, 2 waisawazisha njia ya mtu mnyofu. 1

8Naam, Bwana, tukienenda katika sheria zako, 2 twakungojea wewe, 1 jina lako na sifa zako 2 ndizo shauku za mioyo yetu. 1

9Nafsi yangu yakutamani wakati wa usiku, 2 wakati wa asubuhi roho yangu yakuonea shauku. 1 Wakati hukumu zako zinapokuja juu ya dunia, 2 watu wa ulimwengu hujifunza haki. 1

10Ingawa neema yaonyeshwa kwa waovu, 2 hawajifunzi haki, 1 hata katika nchi ya unyofu huendelea kutenda mabaya 2 wala hawazingatii utukufu wa Bwana. 1

11Ee Bwana, mkono wako umeinuliwa juu, 2 lakini hawauoni. 1 Wao na waone wivu wako kwa ajili ya watu wako tena waaibishwe, 2 moto uliowekwa akiba kwa ajili ya adui zako na uwateketeze. 1

12Bwana, unaamuru amani kwa ajili yetu, 2 yale yote tuliyoweza kuyakamilisha ni wewe uliyetenda kwa ajili yetu. 1

13Ee Bwana, Mungu wetu, mabwana wengine zaidi ya wewe wametutawala, 2 lakini jina lako pekee ndilo tunaloliheshimu. 1

14Wao sasa wamekufa, wala hawako tena hai, 2 roho za waliokufa hazitarudi tena. 1 Uliwaadhibu na kuwaangamiza, 2 umefuta kumbukumbu lao lote. 1

15Umeliongeza hilo taifa, Ee Bwana, 2 umeliongeza hilo taifa. 1 Umejipatia utukufu kwa ajili yako mwenyewe, 2 umepanua mipaka yote ya nchi. 1

16Bwana, walikujia katika taabu yao, 2 wewe ulipowarudi, 2 waliweza kuomba kwa kunongʼona tu. 1

17Kama mwanamke mwenye mimba aliyekaribia kuzaa 2 anavyogaagaa na kulia kwa ajili ya maumivu yake, 2 ndivyo tulivyokuwa mbele zako, Ee Bwana. 1

18Tulikuwa na mimba, tuligaagaa kwa maumivu, 2 lakini tulizaa upepo. 1 Hatukuleta wokovu duniani, 2 hatujazaa watu katika ulimwengu huu. 1

19Lakini wafu wenu wataishi, 2 nayo miili yao itafufuka. 1 Ninyi mnaokaa katika mavumbi, 2 amkeni mkapige kelele kwa furaha. 1 Umande wenu ni kama umande wa asubuhi, 2 dunia itawazaa wafu wake. 1

20Nendeni, watu wangu, ingieni vyumbani mwenu 2 na mfunge milango nyuma yenu, 1 jificheni kwa kitambo kidogo 2 mpaka ghadhabu yake ipite. 1

21Tazama, Bwana anakuja kutoka makao yake 2 ili kuwaadhibu watu wa dunia kwa ajili ya dhambi zao. 1 Dunia itadhihirisha umwagaji damu juu yake, 2 wala haitaendelea kuwaficha watu wake waliouawa.

← Isaiah 25Read In The App, Free →Isaiah 27 →

Study Isaiah 26

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566