Isaiah 15
1Neno kuhusu Moabu: 1 Ari iliyo Moabu imeangamizwa: 2 imeharibiwa kwa usiku mmoja! 1 Kiri iliyo Moabu imeangamizwa, 2 imeharibiwa kwa usiku mmoja! 1
2Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake, 2 mpaka mahali pake pa juu ili walie, 2 Moabu anaombolezea Nebo na Medeba. 1 Kila kichwa kimenyolewa 2 na kila ndevu limeondolewa. 1
3Wamevaa nguo za magunia barabarani, 2 juu ya mapaa na kwenye viwanja 1 wote wanaomboleza, 2 wamelala kifudifudi kwa kulia. 1
4Heshboni na Eleale wanalia, 2 sauti zao zinasikika hadi Yahazi. 1 Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele, 2 nayo mioyo yao imezimia. 1
5Moyo wangu unamlilia Moabu; 2 wakimbizi wake wanakimbilia Soari, 2 hadi Eglath-Shelishiya. 1 Wanapanda njia ya kwenda Luhithi, 2 wanakwenda huku wanalia; 1 barabarani iendayo Horonaimu 2 wanaombolezea maangamizi yao. 1
6Maji ya Nimrimu yamekauka 2 na majani yamenyauka; 1 mimea imekauka wala hakuna 2 kitu chochote kibichi kilichobaki. 1
7Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba 2 wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi. 1
8Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu, 2 kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu, 2 maombolezo yao hadi Beer-Elimu. 1
9Maji ya Dimoni yamejaa damu, 2 lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni: 1 simba juu ya wakimbizi wa Moabu 2 na juu ya wale wanaobaki katika nchi.