Isaiah · Biblia (Kiswahili)

Isaiah 58

1“Piga kelele, usizuie. 2 Paza sauti yako kama tarumbeta. 1 Watangazieni watu wangu uasi wao, 2 na kwa nyumba ya Yakobo dhambi zao. 1

2Kwa maana kila siku hunitafuta, 2 wanaonekana kutaka kujua njia zangu, 1 kana kwamba walikuwa taifa linalotenda lililo sawa, 2 na ambalo halijaziacha amri za Mungu wake. 1 Hutaka kwangu maamuzi ya haki, 2 nao hutamani Mungu awakaribie. 1

3Wao husema, ‘Mbona tumefunga, nawe hujaona? 2 Mbona tumejinyenyekeza, nawe huangalii?’ 1 “Lakini katika siku ya kufunga kwenu, mnafanya mnavyotaka 2 na kuwadhulumu wafanyakazi wenu wote. 1

4Kufunga kwenu huishia kwenye magomvi na mapigano, 2 na kupigana ninyi kwa ninyi kwa ngumi za uovu. 1 Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo 2 na kutazamia sauti zenu kusikiwa huko juu. 1

5Je, hii ndiyo aina ya mfungo niliouchagua, 2 siku moja tu ya mtu kujinyenyekeza? 1 Je, ni kwa kuinamisha kichwa chini kama tete, 2 na kwa kujilaza juu ya nguo ya gunia na majivu? 1 Je, huo ndio mnaouita mfungo, 2 siku iliyokubalika kwa Bwana? 1

6“Je, hii si ndiyo aina ya mfungo niliyoichagua: 2 kufungua minyororo ya udhalimu, 2 na kufungua kamba za nira, 1 kuwaweka huru walioonewa, 2 na kuvunja kila nira? 1

7Je, sio kushirikiana chakula chako na wenye njaa 2 na kuwapatia maskini wasiokuwa na makao hifadhi, 1 unapomwona aliye uchi, umvike, 2 wala si kumkimbia mtu wa nyama na damu yako mwenyewe? 1

8Ndipo nuru yako itajitokeza kama mapambazuko 2 na uponyaji wako utatokea upesi; 1 ndipo haki yako itakapokutangulia mbele yako, 2 na utukufu wa Bwana utakuwa mlinzi nyuma yako. 1

9Ndipo utaita, naye Bwana atajibu, 2 utalia kuomba msaada, 2 naye atasema: Mimi hapa. 1 “Kama ukiiondoa nira ya udhalimu, 2 na kunyoosha kidole na kuzungumza maovu, 1

10nanyi kama mkimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi zenu 2 na kutosheleza mahitaji ya walioonewa, 1 ndipo nuru yenu itakapongʼaa gizani, 2 nao usiku wenu utakuwa kama adhuhuri. 1

11Bwana atakuongoza siku zote, 2 atayatosheleza mahitaji yako katika nchi kame, 2 naye ataitia nguvu mifupa yako. 1 Utakuwa kama bustani iliyonyweshwa vizuri, 2 kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe. 1

12Watu wako watajenga tena magofu ya zamani 2 na kuinua misingi ya kale; 1 utaitwa Mwenye Kukarabati Kuta Zilizobomoka, 2 Mwenye Kurejeza Barabara za Makao. 1

13“Kama ukitunza miguu yako isivunje Sabato, 2 na kutokufanya kama vile upendavyo katika siku yangu takatifu, 1 kama ukiita Sabato siku ya furaha 2 na siku takatifu ya Bwana ya kuheshimiwa, 1 kama utaiheshimu kwa kutoenenda 2 katika njia zako mwenyewe, 1 na kutokufanya yakupendezayo 2 au kusema maneno ya upuzi, 1

14ndipo utakapojipatia furaha yako katika Bwana, 2 nami nitakufanya upande juu ya miinuko ya nchi 1 na kusherehekea urithi wa Yakobo baba yako.” 4 Kinywa cha Bwana kimenena haya.

← Isaiah 57Read In The App, Free →Isaiah 59 →

Study Isaiah 58

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566