Isaiah 25
1Ee Bwana, wewe ni Mungu wangu, 2 nitakutukuza na kulisifu jina lako, 1 kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu 2 umetenda mambo ya ajabu, 2 mambo yaliyokusudiwa tangu zamani. 1
2Umeufanya mji kuwa lundo la kifusi, 2 mji wenye ngome kuwa magofu, 1 ngome imara ya wageni kuwa si mji tena, 2 wala hautajengwa tena kamwe. 1
3Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu, 2 miji ya mataifa katili itakuheshimu wewe. 1
4Umekuwa kimbilio la watu maskini, 2 kimbilio la mhitaji katika taabu yake, 1 hifadhi wakati wa dhoruba 2 na kivuli wakati wa hari. 1 Kwa maana pumzi ya wakatili 2 ni kama dhoruba ipigayo ukuta 2
5na kama joto la jangwani. 1 Wewe wanyamazisha makelele ya wageni; 2 kama vile hari ipunguzwavyo na kivuli cha wingu, 2 ndivyo wimbo wa wakatili unyamazishwavyo. 1
6Juu ya mlima huu Bwana Mwenye Nguvu Zote ataandaa 2 karamu ya vinono kwa mataifa yote, 1 karamu ya mvinyo wa zamani, 2 nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana. 1
7Juu ya mlima huu ataharibu 2 sitara ihifadhiyo mataifa yote, 1 kile kifuniko kifunikacho mataifa yote, 2
8yeye atameza mauti milele. 1 Bwana Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote; 2 ataondoa aibu ya watu wake duniani kote. 4 Bwana amesema hili. 1
9Katika siku ile watasema, 2 “Hakika huyu ndiye Mungu wetu; 2 tulimtumaini, naye akatuokoa. 1 Huyu ndiye Bwana, tuliyemtumaini; 2 sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.” 1
10Mkono wa Bwana utatulia juu ya mlima huu, 2 bali Moabu atakanyagwa chini 2 kama majani makavu yakanyagwavyo kwenye shimo la mbolea. 1
11Watakunjua mikono yao katikati yake, 2 kama vile mwogeleaji akunjuavyo mikono yake ili aogelee. 1 Mungu atashusha kiburi chao 2 licha ya ujanja wa mikono yao. 1
12Atabomoa kuta ndefu za maboma yako 2 na kuziangusha chini, 1 atazishusha chini ardhini, 2 mpaka mavumbini kabisa.