Psalms 10
1Kwa nini, Ee Bwana, unasimama mbali? 2 Kwa nini unajificha wakati wa shida? 1
2Katika kiburi chake, mwovu humtesa maskini, 2 waovu na wanaswe katika hila wanazozitunga. 1
3Hujivunia tamaa za moyo wake; 2 humbariki mlafi na kumtukana Bwana. 1
4Katika kiburi chake, mwovu hamtafuti Mungu, 2 katika mawazo yake yote 2 hakuna nafasi ya Mungu. 1
5Njia zake daima hufanikiwa; 2 hujivuna na amri zako ziko mbali naye, 2 huwacheka kwa dharau adui zake wote. 1
6Anajisemea mwenyewe, “Hakuna kitakachonitikisa, 2 daima nitakuwa na furaha, 2 kamwe sitakuwa na shida.” 1
7Kinywa chake kimejaa laana, uongo na vitisho; 2 shida na ubaya viko chini ya ulimi wake. 1
8Huvizia karibu na vijiji; 2 kutoka mafichoni huwanasa wasio na hatia, 2 akivizia wapitaji. 1
9Huvizia kama simba aliye mawindoni; 2 huvizia kumkamata mnyonge, 1 huwakamata wanyonge na kuwaburuza 2 katika wavu wake. 1
10Mateka wake hupondwa, huzimia; 2 wanaanguka katika nguvu zake. 1
11Anajisemea mwenyewe, “Mungu amesahau, 2 huficha uso wake na haoni kabisa.” 1
12Inuka Bwana! Inua mkono wako, Ee Mungu. 2 Usiwasahau wanyonge. 1
13Kwa nini mtu mwovu anamtukana Mungu? 2 Kwa nini anajiambia mwenyewe, 2 “Hataniita nitoe hesabu?” 1
14Lakini wewe, Ee Mungu, unaona shida na huzuni, 2 umekubali kuyapokea mkononi mwako. 1 Mhanga anajisalimisha kwako, 2 wewe ni msaada wa yatima. 1
15Vunja mkono wa mtu mwovu na mbaya, 2 mwite atoe hesabu ya maovu yake 2 ambayo yasingejulikana. 1
16Bwana ni Mfalme milele na milele, 2 mataifa wataangamia watoke nchini mwake. 1
17Unasikia, Ee Bwana, shauku ya wanaoonewa, 2 wewe huwatia moyo, na kusikiliza kilio chao, 1
18ukiwatetea yatima na walioonewa, 2 ili mwanadamu, ambaye ni udongo, asiogopeshe tena.