Psalms 36
1Kuna neno moyoni mwangu 2 kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. 1 Hakuna hofu ya Mungu 2 mbele ya macho yake. 1
2Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno 2 hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake. 1
3Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, 2 ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema. 1
4Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, 2 hujitia katika njia ya dhambi 2 na hakatai lililo baya. 1
5Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, 2 uaminifu wako hadi kwenye anga. 1
6Haki yako ni kama milima mikubwa, 2 hukumu zako ni kama kilindi kikuu. 1 Ee Bwana, wewe huwahifadhi 2 mwanadamu na mnyama. 1
7Upendo wako usiokoma 2 ni wa thamani mno! 1 Watu wakuu na wadogo 2 hujificha uvulini wa mbawa zako. 1
8Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, 2 nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako. 1
9Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, 2 katika nuru yako twaona nuru. 1
10Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, 2 haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo. 1
11Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, 2 wala mkono wa mwovu usinifukuze. 1
12Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: 2 wametupwa chini, hawawezi kuinuka!